Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » UDOM YAJIPANGA KUJENGA VIWANJA VYENYE UBORA ZAIDI

UDOM YAJIPANGA KUJENGA VIWANJA VYENYE UBORA ZAIDI

Written By mpekuaji on Monday, May 14, 2012 | 9:27:00 AM

makamu mkuu wa chuo kikuu cha dodoma akisalimiana na wanamichezo mbalimabali wakati la bonanza lililofanyika juzi
 
KWA HABARI ZAIDI JUU YA BONANZA HILO ,BOFYA HAPA   <BONANZA>
 
CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM), kina mpango wa kujenga viwanja vya michezo vyenye ubora ili kuweza kukaribisha timu mbalimbali.

Hayo yalisemwa juzi na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idris Kikula wakati wa bonanza la michezo la Profesa Kikula lililofanyika katika chuo hicho mwishoni mwa wiki na kuoingeza kuwa mwaka huu chuo hicho kimefanikiwa kujenga viwanja vipya vya michezo na kilichobaki ni kuwekwa kwa chokaa.

“Michezo ni muhimu sana kwa wanafunzi, tutajitahidi kuwa na viwanja vingi ili wanafunzi wengi zaidi washiriki katika michezo mbalimbali, ikiwemo mpira wa miguu, pete, mpira wa wavu, na michezo mingine,” alisema

Alisema kuwa bonanza la mwaka huu limekuwa na mwamko mkubwa tofauti na mwaka uliopita kwani wengi wamejitokeza kushiriki mashindano hayo na kuwataka wanafunzi kuwa na tabia ya kushiriki katika michezo mbalimbali kwa lengo la kujenga uhusiano mwema na kuimarisha afya .

Mkufunzi wa michezo wa chuo hicho, Patrick Mwani alisema kuwa changamoto wanayokabiliana nayo ni upungufu wa vifaa vya michezo kutokana na chuo hicho kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi ambao wanashiriki michezo.

Katika bonanza hilo, wafanyakazi na wanafunzi wa chuo hicho walishiriki michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, netiboli, mbio za meta 100, mbio za magunia, kufukuza kuku na kuvuta kamba.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts