Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » MAZUNGUMZO YA MALAWI NA TANZANIA KUHUSU MPAKA YAKWAMA

MAZUNGUMZO YA MALAWI NA TANZANIA KUHUSU MPAKA YAKWAMA

Written By mpekuaji on Sunday, August 26, 2012 | 11:28:00 AM


Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Malawi na Tanzania wamesema kuwa mazungumzo kati ya nchi mbili hizo kuhusu mgogoro wa mpaka yamemalizika bila mafanikio na kusisitiza kuwa mazungumzo hayo yataendelea ili kadhia hiyo ipatiwe ufumbuzi. 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Ephraim Mganda Chiume amesema msimamo wa nchi yake ni kwamba, tatizo lililopo litatuliwe kupitia mazungumzo pekee.

 Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe amekiri kwamba kadhia yenyewe ni nzito lakini akaelezea imani yake kwamba itatatuliwa haraka iwezekanavyo. 

Malawi na Tanzania zimefanya mazungumzo kwa takriban wiki nzima kujadili suala hilo. Nchi mbili hizo zinazozana juu ya mpaka wa Ziwa Nyasa huku kila upande ukidai ziwa hilo ni sehemu ya ardhi yake.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts