Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » BIFU LA IDD AZZAN NA SHYROSE BHANJI LAMALIZIKA

BIFU LA IDD AZZAN NA SHYROSE BHANJI LAMALIZIKA

Written By mpekuaji on Monday, May 14, 2012 | 12:44:00 PM

Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan (CCM).
Mbunge Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji.

Lile bifu kiboko lililokuwa likiendelea kati ya Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan (CCM) na Shyrose Bhanji aliyechanguliwa kuwa mbunge Afrika Mashariki hivi karibuni limekwisha

Bifu hilo ambalo lilitokana na mchakato wa kuwania ubunge wa Kinondoni wakati wa kura za maoni katika uchaguzi mkuu mwaka 2010, sasa limeyuka rasmi baada ya waheshimiwa hao kuthibitika kuwa wanapata muda wa ‘kuchati’ na kusalimiana huku Shyrose akikubali yaishe hasa walipokutana kwenye mchakato wa kugombea nafasi ya ubunge wa Afrika Mashariki.

Ilielezwa kuwa hata fomu za kugombea ubunge wa Afrika Mashariki zilikuwa chini ya Azzan hivyo Shyrose hakupata tabu kuzipata.

Mbali na hilo, ilifahamika kuwa Azzan alimtoa woga Shyrose na kumpigia debe, jambo ambalo mwanadada huyo hakuliamini hadi alipopata nafasi hiyo.

Akizungumzia ishu hiyo, Azzan alikiri kumaliza mgogoro huo kwa kumpigia debe hasimu wake huyo hadi akachukua nafasi ya ubunge wa Afrika Mashariki.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts