Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » Esther Wahome awa Mrs Universe Kenya

Esther Wahome awa Mrs Universe Kenya

Written By mpekuaji on Friday, August 3, 2012 | 10:24:00 AM


Muimbaji wa Gospel wa Kenya aliyewahi kutamba na wimbo uitwao ‘Kuna Dawa’ Esther Wahome jumamosi iliyopita alivikwa taji la Mrs Universe – Kenya, kwenye hafla iliyofanyika HiltonHotel, Nairobi.


Mrs Universe ni shindano lililoanzishwa mahsusi kwaajili ya wanawake ‘walioolewa tayari’ na sio kwaajili ya urembo tu bali linalenga kuyaangaza maisha ya wanawake wenye heshima.


Wahome ambaye ni mama wa watoto watatu, ataiwakilisha Kenya kwenye shindano la Mrs Universe August 13, 2012.
Shindano hilo litafanyika nchini Urusi.


Kenya ni miongoni mwa nchi chache zitakazoshiriki kwenye kinyang’anyiro hicho.


Tofauti na Miss World, ambayo huhusisha karibu kila nchini duniani, Mrs Universe ina washiriki chini ya nchi 50.


Kama Tanzania ingekuwa na mwakilishi, unadhani ni nani angefaa kutuwakilisha? Christina Shusho?

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts