Mwigizaji wa picha za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ anadaiwa kukataliwa ukweni na mkwewe wa kike anayefahamika kwa jina la Mama Kigosi au Mama Ray.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, mama Ray hampendi Mainda kiasi cha kutopenda kumuona akifika nyumbani kwake.
“Unajua mama Ray hampendi Mainda, aliwahi kumwambia Ray kuwa, asimuone msichana huyo nyumbani kwake kwani anahisi yeye ndiye anayumbisha maisha ya mwanaye,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya kuipata habari hii ,waandishi wetu walimtafuta Mainda ambaye alikuwa na haya:
"Jamani, jamani hivi ni nani kasema?, kwanza mimi sijawahi kwenda kwa mganga hata siku moja, nimeokoka na siwezi kufanya hivyo.
“Ninajua wanaoleta habari hizo ni Bongo Movies, sijui nimewakosea nini . Ray ananipenda mwenyewe na sijawahi tumia dawa"
Post your Comment


