MSANII wa filamu za Kibongo, Tiko Hassan ameonesha kulikomalia penzi la mume wa mtu na kusema kwamba, yuko tayari kuzaa naye angalau mtoto mmoja.
Akiongea na mpekuzi bila yeye kujua ,Tiko alisema anaumia kuingilia penzi la mwanamke mwenzake lakini kwa kuwa mwanaume huyo anaonesha kumpenda yeye zaidi, bora aambulie hata damu yake tu.
Alisema, katika maisha yake amepita kwa wanaume kadhaa lakini kwa huyo anaona bora atulie na kuyaacha maisha yaendelee.Hajali maumivu anayoyapa mke wa huyo bwana na haimgharimu kwa uchafu huo.
“Choko choko nichokoze, mumeo sikumuita.......
......Huyu ndiye mwanaume niliyekuwa nikimhitaji, ananijali na tangu tumekuwa wapenzi hatujawahi kuwa na ugomvi mkubwa ila wa kawaida tu, hivyo niko tayari kumzalia mtoto mmoja tu,” alisema Tiko.
Post your Comment



