Get the latest updates from us for free

mas template
Home » , » BARNABA AZIDI KUANDAMWA NA MIKOSI......

BARNABA AZIDI KUANDAMWA NA MIKOSI......

Written By mpekuaji on Tuesday, November 27, 2012 | 1:31:00 PM


Msanii Barnaba Elias ameendelea kuandamwa na mfululizo wa mikosi, baada ya wikiendi iliyopita kuibiwa gitaa lake ambalo alipewa na Mke wa Rais wa Marekani aliyopita Mama Laura Bush. Barnaba alielezea kusikitishwa na tukio hilo ambapo anasema liliibwa maeneo ya Leaders nje ya ofisi za THT ambapo ndipo makao makuu ya kituo chao cha kazi.

Akiongea na paparazzi wetu Barnaba alisema, baada ya kuingia katika ofisi za THT siku ya jumamosi, majira ya saa kumi na kumi na mbili na kufanya mambo yake, alishangaa kutolikuta gitaa lake hilo alilopewa kama prize Asset na Laura Bush, Mke wa Rais aliyepita na alichanganyikiwa kidogo kwa namna lilivyotoweka.


“Ninavyokwambia nilifunga milango yote lakini hawa jamaa wametumia mbinu kali maana hakuna mtu aliyeshituka. "


Barnaba anasema bado juhudi za kulitafuta gitaa hilo zinaendelea na anasema atashukuru kama atapata mtu atakayemsaidia kwa taarifa ili kulipata gitaa hilo

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts