Sheikh wa mkoa wa Kagera Haruna Kichwabuta ameliomba Jeshi la polisi mkoani Kagera kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya misikiti ili wawawezeshe waumini wa madhehebu ya kiislamu kushiriki kikamilifu kwenye ibada wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani.
Sheikh Kichwabuta ametoa ombi hilo alipozungumza na waandishi wa
habari ofisi kwake leo,amesema hali ya sasa kwenye maeneo ya nyumba za
ibada sio salama zaidi hasa nyakati za usiku pia ameliomba shirika la
umeme (Tanesco) katika mkoa wa Kagera lipunguze vitendo vya kukata umeme
mara kwa mara kwa kuwa wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani
waumini wa madhehebu ya kiislamu hufanya ibada za usiku.
Aidha amewahimiza waumini wa madhehebu ya kiislamu kutumia mfungo
huo kuimarisha mshikamano kwa hasa kupendana,kusaidiana na pia wawe na
utulivu wakati wa mfungo wa mwezi huo.
Post your Comment


