Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
amesema Taifa lina uhaba mkubwa wa damu salama lakini wananchi hawana
mwamko wa kuchangia damu kwa kuwa hata kama wakichangia wanapokuwa na
wagonjwa hutakiwa kunua nudamu hiyo.
Akizungumza
leo kwenye maadhimisho ya kuchangia damu salama yaliyofanyika kitaifa
kwenye uwanja wa Nyerere Square Mwalimu alisema kuwa tabia ya waganga
Wakuu wa Hospitali za Wilaya na Mikoa kuwauzia damu wagonjwa ndio chanzo
kikubwa kunachopelekea wananchi kutokuwa na moyo wa kuchangia damu.
Ametoa wito kwa waganga wote waliopo kwenye vituo vya afya vya
serikali na hospitali zote za mikoa nchini kuweka mabango yanayoelezea
kuwa damu haiuzwi bali inatolewa bure.
Kwa upande wake meneja wa mpango wa damu salama nchini, Dk, Abdul
Juma amesema kuwa taifa bado lina changamoto kubwa ya uhaba wa damu
salama hali inayohatarisha uhai wa watoto wadogo, akina mama wajawazito
na majeruhi wa ajali mbalimbali.
Post your Comment



