Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » Bodi ya Utalii yasisitiza Mlima Kilimanjaro upo Tanzania

Bodi ya Utalii yasisitiza Mlima Kilimanjaro upo Tanzania

Written By Bigie on Wednesday, July 20, 2016 | 9:54:00 AM

Bodi ya Utalii nchini imetoa taarifa kufafanua kuhusu mlima Kilimanjaro baada ya shirika moja la habari la Marekani kudaiwa kuchapisha taarifa iliyoonekana kuashiria mlima huo unapatikana Kenya.

Taarifa hiyo imekuja baada ya kutokea kwa kifo cha dereva wa kimataifa wa mbio za magari Guguleth Zulu, aliyefariki dunia wakati akipanda Mlima Kilimanjaro.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi ya utalii kwa vyombo vya habari imekanusha taarifa iliyochapishwa na mwandishi wa shirika la AP kwamba milma huo upo Kenya.

‘’Tungependa kusahihisha habari za kupotosha kwamba mlima Kilimanjaro unapatikana Tanzania na si Kenya,”

Aidha Bodi ya Utalii Tanzania imeandika barua kwa chombo cha habari kilichofanya makosa hayo na kutaka wafanye marekebisho.

Miezi michache iliyopita mtoto wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga, Rose Mary Odinga akihutubia vijana nchini Marekani aliwaambia Olduvai Gorge ipo Kenya na baadaye alikanusha taarifa hiyo.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts