Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » Dr Mwaka Kama Ameonewa Aende Mahakamani Ili Sheria Ifuate Mkondo Wake- Waziri Ummy Mwalimu

Dr Mwaka Kama Ameonewa Aende Mahakamani Ili Sheria Ifuate Mkondo Wake- Waziri Ummy Mwalimu

Written By Vuvuzela on Saturday, July 16, 2016 | 8:50:00 AM

 
SEREKALI imemtaka Dk Mwaka kwenda kwenye sheria kama hajaridhika na uamuzi wa serikali  wa kukifungia kituo chake cha tiba za asili.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia,wazee na watoto Ummy Mwalimu wakati akiongea na wadau wa afya katika hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera.

Ummy alisema kuwa uamuzi uliofanywa na serekali wa kukifunga kituo cha afya cha dk Mwaka ni sahihi kwani hajaonewa kwasababu matangazo na huduma alizokuwa akitoa zilikuwa haziendani na maadili na taratibu za udaktari.

"Dk Mwaka asichonganishe wananchi na serekali yao kwamba tumewafungia huduma walizokuwa wakipata kwake wakati huduma alizokuwa akitoa hazikuwa na sifa"alisema Ummy

Alisema kuwa kama anaona ameonewa aende mahakamani ili sheria ifuate mkondo wake."Kama anaona tumemuonea aende mahakamani tutakutana huko"alisema

Waziri ummy Mwalimu yupo Mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo amezindua jengo la wodi ya wazazi iliyojengwa na shirikala jhpiego lenye thamani ya shilingi milioni 150.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts