Baada ya stori za mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda wa Chadema kupewa uzito sana kwenye vichwa vya habari vya magazeti, Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe amezungumza Exclusive na Clouds Media Gruop kuhusu hiyo ishu.
Amesema “vyama vya siasa ni mjumuiko wa watu wengi, wenye uelewa na uvumilivu tofauti hivyo kutofautiana katika vyama vya siasa ni hulka ya kawaida na ni sehemu ya mchakato wa kujenga demokrasia”
Kwenye sentensi nyingine amesema “kwa mantiki hiyo ishu ya Shibuda tutaifanyia kazi kwenye utaratibu tu wa kawaida wa chama, hatuwezi kutoka kwenye track ya kufikiria mambo ya msingi kwa taifa alafu tukaanza kufikiria tofauti za mitizamo kati ya kitengo cha vijana na viongozi mmoja wapo, tutalimaliza kwa wakati, sioni kama linaweza kuathiri chama kwa njia yoyote ile kwa sababu halijagusa misingi ya uwepo wa chama.
Post your Comment


