




Mchungaji wa kanisa la Ufunua Diana Bandele (kushoto) na Abigaili Zumaridi ambaye ni nabii wa kanisa hilo ambao waliwakuta wachawi hao kanisani mwao majira ya saa 12 kwani muda huo ni ada kwa wao kujitakasa kwaajili ya kuianza siku ya ibada.
Ingawa jeshi la polisi linaendelea kuchunguza juu ya hali hiyo, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hakuna kipengele kinacho utambua uchawi hivyo hakuna kesi inayowakabili watu hao.
Watu wawili waliotambulika kwa majina ya Masaganya Kalimanzila (mwanamke, miaka 30) na Chiza Juma (mwanaume) wakihusishwa na imani za uchawi baada ya kubanwa na wananchi, wamekamatwa majira ya saa 12 jana asubuhi katika Kanisa la Ufunuo lililopo maeneo ya Butimba jijini Mwanza wakisafiri kwa ungo (mwanamke) na mshale (mwanaume) kutoka kijiji cha Kaziramkunda, Wilayani Kasulu, Mkoani Kigoma hadi jijini Mwanza, kwa nia ya kuwachukuwa watu watatu walioagizwa.
hizi ni video za tukio zima
hizi ni video za tukio zima
Post your Comment


