Get the latest updates from us for free

mas template
Home » , , » PINDA: BENKI ZITOE RIBA NAFUU KWA WAKULIMA

PINDA: BENKI ZITOE RIBA NAFUU KWA WAKULIMA

Written By mpekuaji on Thursday, May 17, 2012 | 9:18:00 AM

Waziri Mkuu,Mizengo Pinda


WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amezitaka benki nchini kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wakulima  ili waweze kuendelea kilimo.

Pinda alisema hayo jana jijini Dar es Salaam katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Chama cha Kilimo Vijijini Afrika (Afraca).

Katika hotuba hiyo Pinda alisema kwamba, ni muhimu benki hizo zikafika vijijini ili wakulima hao waweze kupata fedha za kuendeleza kilimo chao.

"Wakulima wadogowadogo wanashindwa kupata mikopo ya kutosha kwa sababu benki za biashara zinawatoza riba kubwa na kuhitaji dhamana,"alisema Pinda.

Alisema kutokana na hali hiyo, wakulima hao wamekuwa wakishindwa kupata mikopo kwa kuwa wanaonekana hawawezi kulipa.

"Kutokana na hali hii, taasisi za fedha zijenge uhusiano wa karibu na vyama vya kuweka na kukopa ili kupunguza kukoseka kwa mikopo hasa maeneo ambayo benki hazijafika,"alisema.

Alisema ni matumaini yake kuwa mkutano huo utaangalia jinsi ya kutatua changamoto hiyo ya upatikanaji wa fedha ili sekta ya kilimo iweze kukua.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts