Wakati Bongo Star Search ikitarajiwa kuanza usaili mwezi huu mkoani Dodoma, kampuni ya ShowBiz Defined nayo itafanya auditions kusaka vipaji vya muziki.
Akitoa taarifa hiyo jana, mwenyekiti wa mtendaji wa kampuni hiyo Mike T, amesema usaili huo utafanyika kuanzia tarehe 28-30 mwezi huu.
Vipaji vitakavyosakwa ni vya rap, kuimba pamoja na muziki wa injili.
Mike T amesema shughuli hiyo itasimamiwa na kampuni yake ikishirikiana na Future Sounds Records.
Hata hivyo hakuweza kufafanua kama usaili huo utafanyika pia mikoani.
Post your Comment


