Akizungumza na mwandishi wetu muda mfupi uliopita 'Big Bos' wa kampuni hiyo Said Fella Mkubwa Fella amefunguka kuwa huu ni mwanzo wa mageuzi aliyopanga kuyafanya ndani ya muziki wa kizazi kipya kwa kuwatoa nyota wa kike ambao walikuwa ama hawapewi nafasi sana kama ilivyo kwa vijana wa kiume.
"Kwa mara ya kwanza tunamtoa msanii mdogo wa kike, haya ni matunda ya mipango iliyopo katika kampuni yetu, kam ambavyo mnafahamu tumewatoa wengi lakini wote walikuwa ni wasanii wa kiume, safari hii tumeamua kuweka nguvu kwa wasanii wa kike na tutahakikisha wanapata mafanikio kama ambavyo wanapata wasanii wa kiume, hivyo nawaomba wadau wamsapoti binti huyu ambae tumeanza naye ili kuweka chagizo kwa wasichana wengine kujitokeza na hatimaye tukapata wanamuziki wengi wa kike wenye mafanikio kam ailivyo huko kwa wenzetu. alisema Fella.
hapa chini ni video ya wimbo mpya wa Ching Chilla so cheki nayo halafu utasema nayo
Post your Comment


