Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » BAHATI BUKUKU ANUSURIKA KUPEWA TALAKA BAA

BAHATI BUKUKU ANUSURIKA KUPEWA TALAKA BAA

Written By mpekuaji on Thursday, August 23, 2012 | 11:19:00 AM

Bahati Bukuku.
STAA wa nyimbo za Injili Bongo anayetamba na albamu ya Dunia Haina Huruma, Bahati Bukuku amenusurika kulimwa talaka baa kutoka kwa mumewe waliyetengana naye miaka 7 iliyopita, Daniel Basila.

Kwa mujibu wa chanzo, ishu hiyo ilitokea mwishoni mwa mwezi Julai, mwaka huu ndani ya Baa ya Land Mark Hotel iliyopo Ubungo, jijini Dar.


Ilidaiwa kuwa, Basila alimwita ‘mtalaka’ wake huyo hotelini hapo ampe talaka yake baada ya kuishi ‘singo’ kwa miaka saba huku ndoa yao ikiwa haijulikani hatima yake.


“Daniel alimwita Bahati kwa simu, akamwambia aende pale hotelini akampe talaka. Alipofika alimkuta jamaa ameshika kikaratasi eti ndiyo talaka, lakini Bahati akamwambia kama amedhamiria kutoa talaka aende mahakamani,” kilisema chanzo

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts