Bomba kubwa linalotoa maji bwawa la Mindu kupeleka sehemu ya kutibia maji Mafiga lenye kipenyo cha inchi 24 (24") sawa na milimeta 600 (600mm) limepasuka sehemu mbili tofauti.
Bomba hili ndo linalosambaza maji mjini Morogoro zaidi ya asilimia 75.
Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Morogoro (MORUWASA) inaendelea na juhudi za kulitengeneza bomba hilo kama inavyoonekana kwenye picha ili huduma ya maji ilejee haraka iwezekanavyo.
Shukrani za dhati kwa Rashid Bumarwa kwa kutupatia taarifa hii muhimu

Post your Comment





