Balozi wa China nchini Tanzania ameungana na watanzania katika kuchangia
damu kwa hiari katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwa ni
maadhimisho ya siku ya mchangia damu duniani.
Akiongea
wakati wa shughuli hiyo ya uchangiaji damu Naibu Mkurugenzi wa
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk. Makwiya Makani amesema hospitali
hiyo inakabiliwa na upungufu wa damu kwa asilimia 25.
Dk. Makani ametoa takwimu hizo leo jijini Dar es Salaam
alipomkaribisha Balozi wa China hapa nchini Dk. Lu Youging alipotembelea
hospitalini hapo kwa lengo la kuchangia damu ikiwa ni katika
maadhimisho ya kimataifa ya siku ya mchangia damu duniani.
Dakta Makani amesema kuwa mahitaji halisi ya damu ni chupa 100 hadi
130 kwa siku, lakini chupa zinazopatikana kwa siku ni 60 hadi 100 pekee
ambapo mgonjwa mmoja aliyeafanyiwa upasuaji wa moyo anahitaji
kuongezewa chupa 6 za damu.
Kwa upande wake mkuu wa Idara ya Maabara kuu Dk. Alex Magesa amesema
kuwa hivi sasa ambapo shule zimefungwa na waumini wa Kiislamu wakiwa
katika mfungo,kasi ya kujitolea damu imepungua sana hivyo kunaweza
kutokea upungufu mkubwa zaidi.
Post your Comment




