Msanii mkongwe wa muziki, Mr Nice Jumatano hii aliachia albamu yake mpya ‘Kioo’ ambapo mpaka sasa tayari ameshauza nakala 5000.
Akizungumza akiwa nchini Kenya, Mr Nice amesema albamu hiyo kwa sasa inapatikana nchini Kenya pekee.
“Kama nilivyohaidi kuwa sitembei na single kama wasanii wengine,
natembea kiutuuzima zaidi kwa kutoa albumu,” alisema Mr Nice. “ahadi
nimetimiza na mzigo umeingia sokoni rasmi na tayari nakala 5000
zimenunuliwa fasta ndani ya Kenya pekee,”
Aliongeza, “Nipo Kenya sasa katika tour kubwa kabisa ya kuitangaza
albumu hii mpya na nina zaidi ya mwezi na nusu sasa ni show kwa kwenda
mbele, after Kenya then ni Uganda halafu Rwanda na kwingineko kama
ilivyo kawaida yangu, makoloni yangu yalipo napajua mimi mwenyewe.
Nawashukuru sana mashabiki wa huko nyumbani Tanzania kwa kunisapoti na
kuweza kunitia nguvu na hamasa kwa kipindi chote nilichokuwa nimetulia
nikiandaa mambo na hatimae wakati umewadia na ahadi nimeitimiza sasa,”
Post your Comment



