Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » Rais wa Zanzibar Awaapisha Watendaji wa Serikali hiyo

Rais wa Zanzibar Awaapisha Watendaji wa Serikali hiyo

Written By Vuvuzela on Wednesday, June 29, 2016 | 10:54:00 AM


RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amewaapisha viongozi mbalimbali kushika nyadhifa katika taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

Walioapishwa ni Dk Islam Seif Salim kuwa Naibu Katibu Mkuu, Mifugo na Uvuvi katika Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi. Kabla ya wadhifa huo alikuwa Naibu Katibu Mkuu iliyokuwa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Hassan Abdulla Mitawi ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Habari katika Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo, ambaye kabla ya wadhifa huo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Zanzibar (ZBC).

Aidha, Dk Shein amemuapisha Rafii Haji Makame kuwa Katibu Mtendaji Tume ya Utangazaji Zanzibar katika Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo. Alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) katika wizara hiyo.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts