RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amewaapisha viongozi
mbalimbali kushika nyadhifa katika taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar (SMZ).
Walioapishwa ni Dk Islam Seif Salim kuwa Naibu Katibu Mkuu, Mifugo na
Uvuvi katika Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi. Kabla ya
wadhifa huo alikuwa Naibu Katibu Mkuu iliyokuwa Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Hassan Abdulla Mitawi ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Habari
katika Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo, ambaye kabla ya
wadhifa huo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Zanzibar
(ZBC).
Aidha, Dk Shein amemuapisha Rafii Haji Makame kuwa Katibu Mtendaji
Tume ya Utangazaji Zanzibar katika Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni
na Michezo. Alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) katika
wizara hiyo.
Post your Comment



