Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » Wizkid na Diamond wameipoteza tuzo ya BET kwa Black Coffee, nguli asiyestahili kupuuzwa

Wizkid na Diamond wameipoteza tuzo ya BET kwa Black Coffee, nguli asiyestahili kupuuzwa

Written By Vuvuzela on Monday, June 27, 2016 | 7:35:00 AM


Ushindi wake umeshangaza wengi. Waliokuwa wanatarajiwa zaidi kushinda tuzo hiyo ni Diamond na Wizkid. Na kwa mashabiki wengi wa Diamond, Wizkid ndiye waliyekuwa wakimhofia zaidi. Lakini tulikuja kujipa moyo kuwa huenda mwaka huu ushindi ni wetu kutokana na msimamo wa Wizkid dhidi ya tuzo hizo za Wamarekani. 


Mwaka jana alieleza sababu ya kutohudhuria akidai kuwa haziwapi heshima wasanii wa Afrika na UK. Na tangu atajwe kuwania tuzo hizo, hajawahi kujali,  kusema chochote na hakuhudhuria kabisa. Hivyo nafasi kubwa ilionekana kwenda kwa Chibu. Hata hivyo, BET waliamua kumpa Black Coffee – Dj ambaye jina lake ni geni kabisa kwa Watanzania wengi. 



Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts