Ushindi wake umeshangaza wengi. Waliokuwa wanatarajiwa zaidi kushinda
tuzo hiyo ni Diamond na Wizkid. Na kwa mashabiki wengi wa Diamond,
Wizkid ndiye waliyekuwa wakimhofia zaidi. Lakini tulikuja kujipa moyo
kuwa huenda mwaka huu ushindi ni wetu kutokana na msimamo wa Wizkid
dhidi ya tuzo hizo za Wamarekani.
Mwaka jana alieleza sababu ya kutohudhuria akidai kuwa haziwapi
heshima wasanii wa Afrika na UK. Na tangu atajwe kuwania tuzo hizo,
hajawahi kujali, kusema chochote na hakuhudhuria kabisa. Hivyo nafasi
kubwa ilionekana kwenda kwa Chibu. Hata hivyo, BET waliamua kumpa Black
Coffee – Dj ambaye jina lake ni geni kabisa kwa Watanzania wengi.
Post your Comment





