Mama yake Wema Sepetu, Miriam Sepetu amefunguka kwa kusema anachukizwa
na kitendo cha mwanae kupakaziwa habari ya kuwa ana gonjwa la mapenzi.
Akiongea nasi, Mama Wema amesema akiikumbuka kauli hiyo naumia sana moyo.
“Gonjwa la mapenzi ni gonjwa gani?, wewe mwanao uliyemzaa unaweza
kumwambia ana gonjwa la mapenzi,” alisema Mama Wema kwa ukali. “Hii
kauli imeniumiza sana, watu wake au mashabiki wanaosikia wanatafsiri
nini, binafsi hii kauli imeniuza sana,”
Pia Mama Wema amewataka waandishi wa habari kuacha kuandika habari za kumchafua mwanae bila sababu.
Mama Wema ni mmoja kati ya watu wa karibu wa Wema Sepetu ambao
walihudhia show ya maklia huyo wa filamu ‘The Black Tie’ iliyofanyika
katika ukumbi wa King Solomon weekend iliyopita.
Post your Comment



