Msanii wa muziki wa Hip Hop, Ney wa Mitego amehojiwa kituo cha Polisi Kati na kupewa dhamana kufuatia tuhuma zinazomkabili.
Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema msanii huyo
alihojiwa juzi kituoni hapo na yupo nje kwa dhamana, huku jeshi la
polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.
“Ni kweli juzi mchana tulimhoji Ney wa Mitego na yupo nje kwa
dhamana kuhusu kukamatwa kwake nitatoa taarifa kwa nini
tulimkamata,”amesema Kamanda Sirro.
Hata hivyo, Bongo5 imejaribu kumtafuta rapper huyo wa wimbo ‘Pale
Kati Patamu’ bila mafanikio, kwani kila akipigiwa kupitia simu yake ya
mkononi haipatikani.
Post your Comment



