Get the latest updates from us for free

mas template
Home » » Waliotaka kuzitafuna fedha za tetemeko Kagera wapandishwa kizimbani

Waliotaka kuzitafuna fedha za tetemeko Kagera wapandishwa kizimbani

Written By Vuvuzela on Friday, September 30, 2016 | 4:22:00 PM

Viongozi watatu wa serikali na meneja wa benki ya CRDB, wamefikishwa mahakamani ya Bukoba kwa tuhuma za kula njama kwa kufungua akaunti za bandia inayofanana na ile ya maafa ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera 

Watumishi hao wamepandishwa kizimbani Alhamisi hii mkoani humo huku wakikabiliwwa na mashtaka mawili ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kufungua akaunti feki ya maafa Kagera yenye kesi namba 239/2016.

Waliopandishwa mahakamani ni pamoja na aliyekuwa ofisi tawala mkoa wa Kagera (RAS) Amantius Msole na aliyekuwa mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba, Kelvin Makonda, aliyekuwa mhasibu mkoani Kagera Simbaufoo Swai na meneja wa benki ya CRDB Kagera, Carlo Sendwa.

Wakili wa serikali Hashimu Ngole, alisema watuhumiwa hao wanashtakiwa na makosa mawili, kushirikiana kufungua akaunti feki linalofanana na akaunti ya maafa ya Kagera,na lingine ni kutumia vyeo na madaraka yao kinyume na sheria.

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya

Popular Posts