Kwa sasa headlines nyingi katika upande wa mastaa Tanzania ni stori
kuhusu penzi la muigizaji Jackline Wolper na msanii wa Bongo fleva
kutoka Wasafi Classic Baby (WCB) Harmonize ndio Topic kubwa town.
Katika mahojiano na Take One ya Clouds TV na Zamaradi Mketema, Jackline Wolper ameeleza mambo kadhaa kuhusiana na penzi lake la Harmonize, Diamond ambaye aliwahi kuwa mpenzi wake anachukuliaje mahusiano yao?
“Diamond rafiki yangu sana ni mtu ambae nategemea hata kuja kufanya nae filamu, Diamond ni rafiki yangu sana licha ya watu wanaweza wasielewe, lakini sasa hivi Diamond ni baba mkwe wangu.
“Kuhusu Harmonize nampenda kwa sababu ana hofu ya Mungu, ana heshima
sana mwisho hawezi kufanya maamuzi bila kuomba ushauri, katika kunipenda
mimi alipiatia pia kuomba ushauri kwa Diamond ambaye ni boss wake kaka
yake na kupewa ruhusa kwa hiyo Baraka zimetoka kwa Diamond mwenyewe”
Post your Comment



