Get the latest updates from us for free

mas template
Home » , » AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 31 na 32 )

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 31 na 32 )

Written By Bigie on Friday, March 9, 2018 | 1:17:00 PM


MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA                     
ILIPOISHIA       
“Sawa mkuu”   
Daktari akaongoza nyia, tukafika hadi kwenye chumba ambacho ndipo madkatari wote wanapotakiwa kufika kazini asubuhi wanasaini na pale wanapo toka wana saidi. Raisi akaanza kuligagua daftari hilo, nikaona akitingisha kichwa tu.
“Naombeni koti na mimi leo niwe daktari nikaaa humu kuangali jinsi wanavyo kuja, nyinyi nilindeni kwa nje”
“Sawa mkuu”
Raisi akapewa koti la kidaktari kisha sisi tukatoka nnje ya chumba hichi kuendelea kuimarisha ulinzi. Muda wa kufika ofisini kwa mfanyakazi wa serikali mwisho ni saa moja na nusu tena kwa wale wa mbali ila hadi inafika saa mbili asubuhi hakuna hata mmoja aliye fika, jambo lililo nifanya niwaze sijui ni kitu gani watakacho fanywa na raisi hawa madaktari.

ENDELEA
Tukaanza kuona makundi makundi ya madakatari wakija huku wakitembea kwa mwnedo wa taratibu wakipiga stori kama vile wanakwenda harusini. Hapakuwa NA Daktari aliye weza kustukia ni kitu gani ambacho kinaendelea kwa wakati huu. Hadi wanaingia ofisini humo, ndipo hapo wengine wakagundua kwamba vibarua vyao vipo hatiani kufutwa. Madaktari na manesi si chini ya thelathini wote wamekuja nje ya muda wa kufika ofisini kama mfanyakazi wa uma.
Kutokana na wingi wa wafanyakazi hao hatukucheza mbali na raisi, ambaye amewaitisha kikao cha dharura ndani ya ofisi hiyo hiyo japo wote wamesimama.
 
“Nasemea kuanzia sasa hivi ninavyo zungumza, kazi hamuna”
Sura za manesi na madaktari zikabadilika kila mmoja aliweza kuweka pozi lake, mwenye machozi kumlenga lenga, yalimlenga lenga. Mwenye machozi kumtoka yakamtoka.
“Nyinyi munakuja kazini kama hospitali hii ni ya baba zenu na mama zenu. Daktari mkuu hapa ni nani?”
Mzee mmoja mweusi na mfupi akanyoosha mkono wa kulia.
“Hii hospitali kila mwaka inapata ruzuku ya kiasi gani kutoka serikali kuu?”
“Bilioni tano mkuu”
“Bilioni tano hizo zinatumika katika kufanya nini?”
“Kupaka rangi majengo na…..naa…..naaaaa…..”
Daktari huyo akapatwa na kigugumizi kizito cha kujibu dhairi hawa wanaonekana ndio walaji wa pesa za serikali.
“Hembu huyu muwekeni ndani akajibu hili swala takukuru”
Mlinzi aliyekuja na raisi akamtoa daktari huyo na kumpeleka kwneye magari tulio kuja nayo. Raisi akatoa simu yake na kupiga namba anazo zijua yeye.
 
“Ndio muheshimiwa raisi”
Kila mmoja aliweza kuisikia sauti hiyo kwa manaa raisi ameweka simu yake, loud speaker.
“Una madaktari wangapi wanao ingia makazini wiki hii?”
“Zaidi ya elfu moja mia mbili”
“Hembu niletee madaktari mia moja hospitali ya Bombo hapa Tanga, hadi kesho sijamaliza ziara yangu hapa Tanga wawe wamesha fika”
“Sawa mkuu”
Raisi akakata simu na kuirudisha mfukoni mwake. Akawatazama madaktari hawa na wauguzi kwa macho ya ukali.
“Unajua munapo pewa dhamani na serikali ya kuahudumia watu wake basi musilete longolongo. Saa tatu nyinyi ndio munafika kazini kweli, mimi tangu saa kumi na moja nipo hapa. Nimekuta hospitali ovyo ovyo, ifike kipindi watanzania muelewe kwamba Hapa ni kazi tu na si kuishi kimazoea kama mulivyo kuwa mumezoea kuishi kimazoea”
 
Raisi baada ya kuzungumza hivyoa katokaka na sisi walinzi wake tukamfwata kwa nyuma. Mojo kwa moja tukaelekea naye kwenye gari zetu, nikamfungulia mlango, akapanda nikaingia upande wa dereva na kuondoka eneo la hospitali huku tukiacha watu ambao wamemuona raisi kila mmoja akiwa anazungumza lake.
“Nipelekeni soko la Ngamiani”
“Sawa muheshimwa”
Simu ya muheshimiwa ikaita, akaitoa mfukoni, akaipokea na kuiweka sikioni mwake.
“Ok”
“Nyinyi tu nendeni kwenye uwanja wa hapo Mkwakwani”
“Hawawezi kukujua, mimi naendeleza ziara yangu”
“Ulinzi uzidi kuimarishwa”
“Ok”
Raisi akakata simu, tukaelekea moja kwa moja kwenye soko la Ngamiani, mazingira ambayo tumekutana nayo hayakunistajabisha sana kwa maana ninalifahamu soko hili kwa uchafu. Wafanya biashara wakabaki wakiwa wamejawa na kigugumizi kwa maana wanatambua raisi yupo katika uwanja wa Mkwakwani kwa ajili ya kuzungumza na wananchi ila wanamuona huku sokoni muda huu. 
 
“Habari zenu?”
“Salama muheshimiwa”
“Naona bishara zinakwenda?”
“Zinakwendaje muheshimiwa, wakati watoza ushuru wakatoza bei kubwa kila siku bei inapanda”
Mfanya bishara mmoja alizungumza kwa sauti ya uchungu iliyo jaa gadhabu.
“Ehee, wanawatuza shilingi ngapi?”
“Muheshimiwa imtoka shilingi mia mbili hadi mia tano kwa kila kichwa kwenye hili soko”
“Na mbona mazingira ni machafu?”
“Ndio hapo sasa muheshimiwa, manispaa wanatunyanyasa sana, kwanza hawaji kufanya usafi, pili wanadai ushuru unapanda kwa ajili ya kodi unayo sema muheshimiwa”
Wafanya bishara hao wakatoa malalamiko yao kila mmoja kwa wakati wake, raisi hakusita kuyaandika malalamiko hayo kwenye kijikitabu chake cha kumbukumbu. Akawaaga wafanya bishara na tukaondoka katika soko hili.
 
“Hii Tanzania bwana, kiongozi wa juu anamuambukiza kiongozi wa chini madudu, huku nao wa chini wanafanya utumbo, ila mwaka huu watanijua mimi vizuri”
Raisi alizungumza huku tukiwa ndani ya gari, tukielekea kwenye gereza la Maweni. Ni ngumu sana kwa mtu kuweza kutambua kwamba raisi tupo naye sisi kwenye hizi gari mbili, huku gari la baba mkubwa, likitufwata kwa nyuma. Tukafika kwenye gereza la Maweni huku tukiwa na daktari mkuu. Akashuka mlinzi wa niliye kuwa naye ndani ya hili gari, akamfwata askari aliye simama kwenye nje ya kibanda kilichopo hapa getini cha kuingilia eneo la gereza hili. Akazungumza naye maneno mawili matatu, geti likafunguliwa, gari zetu zikaingia. Moja kwa moja tukaeleka katika ofisi ya mkuu wa gereza, kwa bahati nzuri tukamkuta. 
 
   Alipo muona rahisi, wasiwasi mwingi uliweza kumjaa, raisi akaachia tabasamu pana na kumsalimia mzee huyu aliye valia nguo za askari magareza.
“Mzee mbona una wasiwasi?”
“Kusema kweli muheshimiwa sijategemuea kama unaweza kuja eneo hili”
“Unaogopa?”
“Aaha hapana”
“Nahitaji kuonana na wafungwa wote nao nataka kusikia maoni yao”
“Sawa”
Mkuu wa gereza akatoa amri kwa kijana wake, aende akaandae mazingira ya raisi kuweza kuoana na raisi.
“Twende tu, hakuna haja ya kuandaa mazingira nahitaji kuona jinsi wafungwa wanavyo ishi”
 
Ikabidi kijana huyo ambaye nayepia ni askari magareza kusitisha safari yake hiyo ya kwenda kuandaa mazingira mazuri ila hata raisi akienda asione mabadiliko. Tukafika kwenye moja ya uwanja ambo ni maalumu kwa mazoezi ila kitu tulicho kikuta kila mmoja alishangaa, ikatubidi sote wanne kuweza kuchomoa bastola zetu na kuziweka tayari kwa lolote litakao tokea. Kwanza uwanja huu umelowana kwa maji mengi yaliyo sababisha tope jingi. Wafungwa zaidi ya mia moja, wanapigishwa mazoezi makali huku wakiwa na vijibukta tu, sura zoa wala huwezi kuziona vizuri kwa kujaa damu kwani askari gereza wanawapiga kwa vitako vya bunduki wale ambao wanaleta ubishi katika kutekeleza kile ambacho askari hao wamekiamrisha.
 
Raisi akamtazama mkuu huyu wa gereza ambaye mwili mzima unamtetemeka kwa woga kwa maana mafunzo wanayo yatoa hapa ni mafunzo ya kijeshi, ina maana kuna mpango mkubwa unao fanywa na wakuu hawa wa gereza kupitia wafunga hawa ambao hawawathamini kama binadamu.
“Hivi ni macho yangu au nina ota?”
Raisi alizungumza huku akiendelea kutazama wafungwa hao jinsi wanavyo pewa mazoezi makali, ata askari wanao fanyisha mazoezi hayo hawakuweza kujua ni kitu gani kinacho endela, wao kwa sifa wakazidi kuwashushia kipigo wafungwa hawa.
“Wanafanya mazoezi kwa ajili ya nini?”
“Ahaa….mu…mu….heshiii miwaaa. Unajuaa nini?”
“Nini?”
“Nchi hii kidogo ulinzi umeyumba yumba na sisi tunaandaa vijana wetu wame wakakamavu”
“Wakakamavu wafungwa, wamekuja huku  muwafundishe maisha bora ya kuja kuishi uraiani, nyinyi mutafundisha waje kuwa majambazi. Amrisha watu wako kuacha zoezi hili mara moja”
 
Hapo ndipo nikamuona raisi akiwa amezungumza kwa kukasirika, huku akiiweka weka vizuri miwani yake sawa. Mzee huyo hata sauti haikumtoka, ikambidi kijana wake kumsaidia kutoa sauti ya ukali iyo wafanya askari magereza hao kuacha kile wanacho kuifanya. Wafungwa hawa miili yao imezohofika kwa njaa na mateso wanayo yapata. Askari magereza walio kuwa wanendesha mazoezi hayo walipo gundua kwamba raisi yupo hapa waliishiwa pozi kabisa kila mmoja alijihisi anavyo jisikia yeye.
“Nani ametoa hili agizo la kuwafundisha mazoezi ya kijeshi?”
“Ahaaa muhe…..”
“Sitaki kusikia muheshimiwa, ni nani ametoa agizo hili”
“Ni mkuu wa mko mzee”
“Ahaa yeye ndio anaye badilisha amri ya nchi?”
“Ahaaa”
Raisi akaanza kuelekea katika uwanja huu, mimi na Babyanka hatukumuacha kusonga mbele, bado bastola zetu zipo mikononi, na tukimtazama kila aliye karibu na raisi.
“Habari zenu”
 
“Sala..maa”
Wafungwa wachache waliweza kuitikia ila wengine walishindwa kasisa kufanya hivyo kutokana na kuchoka kwa kipogo kikali wanacho kipata.
“Munafundishwa juu ya nini?”
“Muheshimiwa bora yaani umekuja, sisi wengine humu tumefungwa kwa kesi za kusingiziwa, ila tumekuja huku tunakutana na mateso makali kama haya”
“Yana muda gani?”
“Miezi mitatu sasa, kuna wezetu wachache kila siku usi……”
Mfungwa aliye kaa karibu na mfungwa huyu anaye zungumza akamuwahi mwenzake na kumfunga mdomo kwa nguvu. Mfungwa huyo aliye zibwa mdomo akampiga mwenzake kisukusuku cha kifua na kusababisha vurumai kuanza kutokea, kati ya wafungwa hao, jambo lililo tufanya mimi na Babyanka kuchanganyikiwa tukitafuta ni jinsi gani tunaweza kumuokoa raisi kutoka katikati ta watu hawa wanao onekana kujawa na hasira kali sana.
                                                                                         
                         AISIIIII……….U KILL ME 32

Babyanka akapiga risasi mbili hewani na kuwafanya wafungwa wote kulala chini huku wakivifunika vichwa vyao.
“Muheshimiwa tuondoke”
Nilimuambia raisi huku nikihakikisha kwamba anakuwa salama muda wote, raisi akakubaliana na ombi langu kwa maana hali sio salama kabisa katika eneo hili. Tukampeleka raisi hadi kwenye ofisi tulizo kuwepo awali, huku mkuu wa gereza akiwawa kimya kabisa. Ukimya ukatawala ndani ya ofisi huku kila mtu akiwa kimya. Raisi akatoa  simu yake ya mkononi, akaminya baadhi ya batani kisha akaiweka sikioni.
“Andaa jeshi kudhibiti sekta zote za ulinzi”
 
“Hakikisha kwamba, mkuu wa mkoa pamoja na kundi lake munawaweka chini ya ulinzi mkali”
“Pia nahitaji vijana watakao linda hili gereza kuanzia sasa hadi pale nitakapo toa tamko jengine”
Raisi akakata simu, huku akionekana kuwa na hasira kali sana, akamsogelea mkuu wa gereza akabandua vyota zilizopo begani mwake ikiashiria kwamba amevuliwa cheo.
“Mkamate bosi wako kamsweke ndani”
“Sawa muheshimiwa”
Kijana wa mkuu wa gereza akamchukua aliye kuwa mkuu wa greza huku akimpiga pingu na kuondoka naye katika eneo la ofisini. Raisi kwa ishara akamtuma mlinzi mmoja kwamba afwatile hadi mkuu huyo atakapo wekwa ndani.
“Tuondokeni”
 
Kazi yetu ni kufwata amri ya raisi, tukaongoza njia, huku mbele nikitanguli mimi, nyuma akifwata Babyanka pamoja na mlinzi mwengine ambaye hasi sasa hatujajuana majina kabisa kutukana na mihangaiko ya kazi yetu hii. Tukaingia kwenye magari na kuondoka katika eneo la gereza hadi tunafika barabarani, raisi hakuzungumza kwamba ni wapi tuelekee.
“Muheshimiwa mbunge yupo  wapi?”
Swali la raisi, likanifanya kusimamisha gari kwa maana hata wazo la kumtazama mama na baba mkubwa ambao tuliingia nao hapo gerezani, lilinipotea kabisa.
“Mbona umesimamisha gari?”
“Sifahamu kwamba tumewaacha wapi muheshimiwa kwa maana tangu tuelekee kwenye uwanja wa wafungwa hatujawaona”
Raisi akatoa simu mfukoni mwake na kumpigia baba mkubwa Eddy, ila akaishusha simu hiyo kama sekunde kumi baada ya kuiweka sikioni. Akairudisha tena sikioni, akaishusha tena kwa muda mchache huo huo.
 
“Hapatikani?”
“Hapatikani?”
“Ndio”
“Ninakuomba nikawaangalie muheshimiwa”
Raisi akaka kimya kwa sekunde kadhaa akionekana kulifikiria ombi langu.
“Hapana tuendelee na safari, nimetuma vikosi vya jeshi vitakuja kuimarisha ulinzi katika eneo hili”
Sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea na safari ya kuelekea Tanga mjini, akilini mwangu muda wote nikawa ninamfikiria mama na baba mkubwa huku nikijiuliza wamepotelea ndani ya gereza hilo au laa, kwa maana vurugu za wafungwa wale ninaimani zimeweza kuwatisha. Simu ya muheshimiwa raisi ikaita. Akaipokea kwa haraka na kuiweka sikioni mwake.
“Mumefanikiwa?”
 
“Sasa washikilieni hadi niwakute”
Akakata simu na kunipa maelekezo nielekea kwenye mji wa Sahare.
“Spidi mia na ishirini”
“Sawa”
Nilimpa Babyanka amri ya kuongeza mwendo kasi wa gari zetu kwa maana tunahitaji kuweza kudfika katika eneo hilo la Sahare ndani ya dakika kumi. Barabara ziliweza kutawaliwa na trafiki ambao wanaimarisha ulinzi wa baba bara hiyo wakiamini raisi aliyopo katika uwanja wa Mkwakwani ni raisi kweli kumbe ni raisi feki. Kila trafki aliye simamisha gari letu aliishia kuisima namba ya gari, hatukupunguza wala kuhofia kitu chochote, huku mimi ndio nikiwa ninauongoza msafara huu. Tukafanikiwa kufika eneo la Sahare. Tukaelekezwa hadi sehemu ya tukio ambayo ninaifahamu kabisa, ni sehemu ya jumba ambalo lilikuwa linatumiwa na Meya kuhifadhia wapiganaji wa Al-Shabab.
 
“Tukashuka kwenye gari huku tukuwa makini, tukaingia kwenye jumba hili huku tukiwa makini sana, tukakutana na wanajeshi si chini ya kumi wakiwa na silaha za kivita, wakiwashikilia wapiganaji wote waliokuwa ndani ya jumba hili wapatao hamsini.
“Mumewashika vipi?”
“Walikuwa ndio wanajiandaa kugawanyika katika kwenda kuvamia mkutano wako”
“Mukiwahoji wana kitua ambacho wanakizungumza?”
“Hapana hakuna kitu ambacho wanakizungumza?”
“Silaha zao mulizo wakamata nazo zipo wapi?”
“Hipo huku”
 
Mkuu huyo wa oparesheni ya kimya kimya alizungumza na raisi, na kuanza kuongozana naye kwenda kumuonyesha silaha hizi sehemu zilipo, sisi tukafwata kwa nyuma. Tukakuta silaha nyingi pamoja na mabomu vikiwa vimetandazwa chini, huku kukiwa na wanajeshi wengine wapatao sita wakiwa wameimarisha ulinzi sehemu hiyo.
“Aisee hawa watu, dawa yao ni kufa kabisa”
“Muheshimiwa, si tungewarudisha kwao na wakahukumie huko?”
“Huko kwao wenyewe wanashindwa kuwahukumu, sasa nahitaji wote wafe mbele yangu”
Amri ya raisi, hakuna ambaye anaweza kuipinga zaidi ya kuitelekeza. Tukarudi katia sehemu walipo shikiliwa wapiganaji hao. Wakaamrishwa kupanga mistari miwili, wakafanya hivyo huku wengine wakiwa wanavuja damu, wakionekana kushushuwa kipondo kikali kutoka kwa wanajeshi hawa wanao onekana kuwa ni makombandoo.
 
Walipo maliza kupanga mstari, kila mwanajeshi, akaifunga bunduki yake kiwambo cha kuzuia risasi na hata kama wakipiga risasi mtu aliyeyopo nje ya jumba hili wala hatasikia chochote. Ikatolewa amri ya kijeshi ya kujiandaa, kisha ikatolewa amri ya kushambulia. Milili ya wapiganaji wa kikundi hichi cha Al-Shabab, wakaanza kudondoka mmoja baada ya mwengine huko wote wakiwa wametandikwa risasi zakichwa. Kwa mara yangu ya kwanza katika maisha yangu, ndio ninashuhudia maujia ya watu wengi kiasi hichi, japo jana usiku niliweza kufanya kazi ya kuwaua wapiganaji wengine ila hii ya leo inatisha sana.
“Maiti zao hakikisheni kwamba munazitupa baharini mbali, ambapo hakuna mtu anaye weza kuziona wala kujua ni kitu gani ambacho kimetokea”
“Sawa mkuu”
 
“Je kuna kingine ambacho kimetoke?”
“Kama ulivyo agiza mkuu wa mkoa tayari yupo chini ya ulinzi, anahojiwa kambini huko”
“Ok hakikisheni kwamba kila kitu kinakwenda kama vile nilivyo agiza”
“Sawa mkuu”
Tukaondoka na raisi namoja kwa moja tukaelekea katika uwanja wa Mkwakwani, ambao umejaa wananchi wengi watanga wakimsikiliza raisi feki akitoa hotuba aliyo iandaa raisi tuliye kuwa naye.
“Amefanya vizuri”
Raisi alizungumza huku akiwa ndani ya gari hapakuwa na mtu aliye weza kushuka. Simu ya raisi ikaita, akaipokea.
“Ndio  muheshimiwa mbunge?”
“Mupo salama lakini?”
“Sawa”
Raisi akakata simua na kuirudisha simu yake mfukoni.
“Mama yupo salama”
“Shukrani muheshimiwa”
 
“Sasa safari ya kurudi Dar es Salaam itaanza sasa, nitaondoka na vijana nilio kuja nao na nyinyi jichanganyikeni katika raisi huyu murudi naye kesho”
“Sawa mkuu”
“Nimesha mtumia picha zenu kwa hiyo atawatambua pasipo nyinyi kujitambulisha”
“Sawa mku”
Nikashuka kwenye gari na kumuacha kijana wa raisi akiingia kwenye upande wangu wa dereva, huku kijana mwengine akishuka kwenye gari la Babyanka na kuingingia kwenye gari nililo shuka mimi, huku na mimi nikielekea kwenye gari la Babyanka. Raisi na vijana wake wawili wakandoka na kutuacha mimi na Babyanka uwanjani hapa.
“Nina usingizi ile mbaya”
“Wewe una nafuu, mimi hapa nilikuwa ninaendesha gari huku nasinzia sinzia, afadhali sijamuendesha raisi”
“Daa tupate ata kamuda kakulala”
“Sasa hatujajua raisi huyu naye anaondoka hapa uwanjani saa ngapi”
“Ngoja nishuke nitafute ratiba yake.”
 
Nikashuka kwenye gari huku nikiwa makini, nikatazama walinzi wengine walio zagaa kila kona ya uwanja huu wakiimarisha ulinzi, huku walinzi wengine wakiwa hawafahamu kwamba raisi waliye kuwa naye sio raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, kwani raisi mwenyewe alisha ondoka na huyu amevaa tu kinyago kinacho fanana na raisi wetu.
“Kaka habari”
“Safi”
Nikamuonyesha mlinzi huyu kitambulisho changu, akakisoma vizuri, kisha akanirudishia.
“Raisi akitoka hapa anaelekea wapi?”
“Anaeleka mkonge Hotel kupumzika usiku atapata chakula na wazee wa jiji hili”
“Ok asante”
“Ila mbona unauliza kama ni mgeni wa hii ratiba?”
“Hapana mimi muheshimiwa alipa kazi ambayo ndio nimeimaliza muda huu”
“Ahaa sawa”
Nikaachana na mlinzi huyu ambaye alianza kunitilia mashaka, nikaingia kwneye gari na kuufunga mlango.
 
“Anasemaje?”
“Akitoka hapa anelekea Mkonge hoteli”
“Twende tukatafute sehemu tulale aisee”
“Poa”
Babyanka akawasha gari, tukaondoka eneo hili la hotelini moja kwa moja tukaeleka kwenye hoteli ya Maua INN, kwa maana ndio sehemu ya pekee ambayo si raisi kwa watu kutustukia kwamba sisi ni walinzi wa raisi, japo hoteli hii ipo kaikati ya mji ila imetulia sana.
Tukafika katika eneo hili, tukasimamisha gari letu kwenye maegesho akaanza kushuka Babyanka akaingia ndani, akalipia chumba na moja kwa moja akelekea sehemu kilipo na kwa kupitia kifaa cha mawasiliano akaniambia ni chumba namba ngapi yupo, nikashuka kwenye gari na kufunga milango vizuri, moja kwa moja nikaelekea kwenye chumba hicho, wala sikumsalimia muhudumu wa hii hoteli aliye kaa mapokezi. Nikapandisha gadi gorofa ya nne na kuingai katika chumba alicho nieleza Babyanka. Nikamkuta akiwa amelala kitandani na nguo zake pamoja na viatu vyake huku bastola yeka ikiwa pembeni yake.
 
“Dany mskaji wangu hembu naomba ukanichukulie maji nina kiuu”
“Ahaa si upige simu?”
“Ahaa sitaki wahudumu kujua jua chumba tulichopo”
Kutokana sikuwa nimekaa sehemu yoyote nikageuza na kutoa chumba huku nikiufunga mlango wa chumba vizuri. Nikaanza kutembea kwenye kordo hii huku nikiwa makini kutazama nyuma na mbele. Mlango wa chumbani cha mbele ukafunguliwa, ikanibidi kupunguza mwendo  wa kutembea, macho yakanitoka baada ya kumuona K2 na Lukas wamesimama mlangoni hapo huku wakipigana mabusu ya mdomoni, huku Lukas akiwa amejifunga taulo kiunoni na K2 akiwa amevalia suti yeusi, ila vifungo vya shati lake vikiwa havikajaa vizuri, kwa bahati mbaya, K2 akanitazama, kitu kilicho mstua sana hata Lukas naye alivyo niona akakimbilia ndani.
                                                                                          ITAENDELEA

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya