MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
0657072588
0657072588
ILIPOISHIA
Hata kabla Vivia hajanijubu chochote, mlango huu ukaanguka chini baada ya kuvunjwa kwa nguvu. Kundi kubwa la wasichana hawa wakijeshi wakiwa wameongozana na mkuu wao wa hili gereza wakasimama mlangoni, huku nyuso ya huyu mwana mama mkuu wao ikiwa imetengeneza alama ya ‘V’ kutokana na hasira kali aliyo nayo. Vivian na wezake wakajikuta wakikurupuka kila mmoja akajawa na wasiwasi mwingi sana kwani kinacho kwenda kutokea Ahmood alisha wahi kuniambia.
ENDLEA
Mama huyo akawaamuru wanajeshi wengine kuwakamata wezao ambao wote wapo uchi, haya mimi mwenyewe nipo kama nilivyo zaliwa. Vivian alipo karibiwa kukamatwa na mwenzake mmoja, akaanzisha varangati, jambo lililo nipa hata mimi nguvu. Wezake wengine nao watatu kazi ikawa ni kupambana na hawa wanajeshi wezao.
Japo tupo uchi wa mnyama wala hatukulijali hilo, kikubwa hapa ni kila mtu kuyaokoa maisha yake. Hapa ndipo nilipo gundua kwamba wasichana hawa mapigano yao hayana tofauti kabisa na wasichana wa Livna.
Vivian hakuwa mbali na mimi, kila msichana ambaye alihisi anaweza kunizidi aliweza kumdhibiti kisawa sawa. Tulipo pata upenyo wakutoka katiki hichi chumba kilicho jaa damu nyingi, tukatoka na kuanza kukimbia hivyo hivyo tulivyo. Vivian akawa na kazi ya kuniamrisha nimfwate nyuma. Kutokana taa zimewashwa na ving’ora vimepigwa kila sehemu, haikuwa rahisi kwetu sisi kuto kuona tunapo elekea. Tukaingia kwenye moja ya chumba ambacho ni cha kuhifadhia nguo za wanajeshi hawa.
“Chagua haraka haraka nguo itakayo kutosha”
“Poa”
Nikaanza kuchambua suruali ambazo zinaweza kunienea, kwa habatiu nzuri sikupata shida kabisa, nikapata moja ya suruali ambayo imeniendelea vizuri. Nikaikavaa na kufunga zipu pamoja na vifungo chake, nikatafuta na shati la juu ambalo nalo pia ni la kijeshi, nikavaa.
“Chukua viatu hivyo”
Vivian alinirushia buti za kijeshi huku akiwa anamalizia na yeye kuvaa.
“Hivi unafahamu njia ya kutokea humu ndani?”
“Yaaa ninaifahamu ila ni ya hatari kubwa sana, ni heri kwenda kufia huko mbele ya safari kuliko kukamatwa na huyu jinni. Kifo chake ni kibaya sana”
“Mmmmm”
“Tuondoke”
Vivian alizungumza huku akiusogelea mlango, akausukuma taratibu na kuchungulia nje, sikujua ameona kitu gani, kwa ishara akaniomba nirudi nyuma, tukajificha kwenye moja ya kabati kubwa. Wakaingia wasichana wawili wakiwa na silaha, wakaanza kuchunguza taratibu ndani ya hichi chumba. Vivian akanipa ishara ya kwamba kila mmoja apambane na wakwake. Ndivyo ilivyo kuwa pale wasichana hawa walivyo jaribu kulisogelea kabati tulilo jificha, kilicho wakuta, mi Mungu tu ndio anaye jua, kwa maana kila mmoja alimuua wa kwake kwa staili anayo ijua yeye. Tukazidi kujiamini sana baada ya kuzipata bunduki zao, Vivian akakimbilia mlangoni akachungulia nje kwa mara nyingine, kwa ishara akaniita hadi mlangoni na tukatoka na kuanza kukimbilia nje.
“Tupite huku”
Vivian alizungumza huku akikunja kushoto, tukazidi kusonga mbele kwenye njia ambazo ndio mara yangu ya kwanza kuziona ndani ya hili gereza.
“Dany kuwa makini huku tunapo pita ni njia ambayo kunafugwa majoka makubwa sana na tusipo kuwa makini tutafia huko”
Vivian alizungumza huku jasho jingi likimwagika usoni mwake, nikajikuta nikishusha pumzi kusema kweli, mbele ya majoka haya hakuna mtu ambaye anaweza kuwa jasiri kwa maana majoka hayo anayo yazungumza Vivian sijui hata yanafananiaje.
Viviana akafingua moja ya mfuniko wa chuma ambao upo chini ya ardhi. Akanitazama tu usoni mwangu, kisha akanisogelea na kuninyonya lipsi zangu kwa nguvu sana, huku akishusha pumzi nyingi sana.
“Kama tukifa tutakuwa tumeondoka kihaki kwenda kwa mwenyezi Mungu na kama tukibahatika kupona pia ni bahati ya mola”
“Kweli”
“Kwenye sehemu ya hayo majoka tunatakiwa kupita kimya kimya, kijimlio chochote kikitokea basi tutakuwa chakula cha hayo makoka”
“Sawa”
Nilizungumza huku nikishusha pumzi, nikajaribu kuchungulia ndani ya shimo hili refu. Huko tunapo kwenda hakuna mwanga wa aina yoyote. Roho moja inaniambia ni bora ni baki nijisalimesha mikononi mwa mama huyu ila roho nyingine inaniambia nikimbie na hii ndio nafasi yangu ya pekee katika kuyaokoa maisha yangu.
“Twende”
Vivia alizungumza huku akivaa mkanda wa bunduki ambayo inaning’inia mgongoni mwake, na mimi nikauvaa mkanda wa bunduki yangu, kisha nikamshubiria Vivian azame kwenye shimo hilo lenye giza totoro. Baada ya Vivi kuzama na mimi nikazama na kuanza kushuka kwenye ngazi hizi. Kusema kweli kuna maeneo yanatisha duniani, na unaweza kwenda kuzimu hata kabla hujafa. Kwenye vitabu vya dini tunaelezwa kuzimu ni sehemu yenye giza nene, ambalo kwa haraka haraka ninalifananisha na hii sehemu tunayo shuka.
“V”
Niliita kwa sauti ya chini sana chini ya kunong’oneza.
“Mmmmm”
“Sioni tunapo kwenda”
“Tunashuka chini tu, hadi tukute mwanga”
“Na hizi ngazi?”
“Ndio hapo chini chini ndio kuna hayo majoka”
“Mungu asaidie”
“Ngazi ya hamsini ndipo kuna hayo majoka na hadi sasa hivi mimi nipo ngazi ya ishirini”
“Na ngazi zipo ngapi?”
“Zidi ya miambili na hamsini”
Tulizungumza kwa sauti ya chini sana, tukaendelea kushuka taratibu na giza latu totoro. Kila jinsi tunavyo zidi kushuka chini ndivyo hali ya hewa inavyo zidi kubadilika, ikafikia hatua hewa ikawa mbaya sana. Nikaanza kuhisi maumivu makali ya kichwa jambo lililo anza kunipa woga mkubwa. Jasho jingi likaanza kutiririka katika mwili wangu, joto kali lisilo na kifani, nalo kitatawala mwili wangu.
“V”
“Shiiii”
Sauti ya Vivian nayo imebadilika kabisa, kwa haraka nikaanza kuhisi na yeye anaipitia hali ambayo ninayo mimi. Harufu kali ya uozo ikatawala katika pua zangu, nikajua eneo tulilopo ndio eneo ambalo hayo majoka yanafugwa. Tukaanza kusikia mihemo mizito na yakutisha, nikahisi kufa ila malaika mtoa roho amekaa mbali na mimi.
Nilicho kikremisha ni jinsi ya kushuka kwenye gazi hizi ndefu kwenda chini. Vivian aliyopo chini yangu wala sikumsikia hata ishara yoyote. Taratibu nikshusha mguu wangu hadi kwenye ngazi ya chini yangu, ila nikahisi nimekanyaga kiganja cha Vivian. Kwa haraka nikaurudisha mguu wangu kwenye ngazi niliyopo huku mikono yangu ikiendelea kushikilia ngazi ya juu. Hali ya kuumwa ikazidi kunitawala mwilini mwangu, nikatamani kujiachia, ila ninashindwa, ninatamani hata muujiza ujitokeze niokoke kwenye hili eneo ila hakuna kitu kama hicho.
Tukaendelea kushuka kwa umakini mkubwa sana katika eneo hili la kutisha, cha kumshukuru Mungu hatuyaoni hayo majoka nalaiti kama tungekuwa tunayaona nahisi ni siku nyingi tungekuwa tumesha liwa kutokana na woga wa kibinadamu. Tukazidi kushuka chini kwa kujikaza japo nguvu za mwili zimetuishia ila hakuna jinsi zaidi ya kuendele kujikaza tena zaidi ya ukakamavu. Kadri tunavyo zidi kushuka ndivyo hali ya hewa inavyo anza kubadilika, ikafikia hatua miili yetu ikaanza kupata unafuu ambao kusema kweli matumaini ya masiha yetu kuokoka yapo. Tukafika sehemu hali ya hewa ambayo tumeizoea ikatawala katika mifumo yetu ya kuhemea.
“Dany”
“Mmmm”
“Tumeokoka”
“Kweli?”
“Ndio naamini sisi ndio tutakuwa wa kwanza kuokoka kutoka katika hili gereza”
“Ila mbona sioni huo mwanga”
“Tukifika ngazi ya chini kuna sehemu ya kutembea kama dakika ishirini na ndio tutakuta geti la kutokea”
“Sawa”
Kweli tukafanikiwa kufika ngazi ya chini, tukaanza kutembea kuufwata ukuta huu, kila tunavyo zidi kwenda ndivyo tunavyo hisi kupanda juu kwani sehemu hii ni kama ya muinuko. Wasiwasi wote ukaniishia moyoni mwangu na furaha kubwa ikaanza kunitawala moyoni mwangu. Kama Vivian alivyo zungumza ndivyo jinsi ilivyo, kwani dakika ishirini nzima zikaisha tukiwa katika kutembea katika eneo hili.
Tukakuta geti la nondo za chuma, kufuli kubwa lililopo katika geti hili halikutuangaisha sana kwa maana tuna bunduki zenye risasi za kutosha. Mwanga wa mbalamwezi unao angaza nje ukazidi kunipa kiweluwelu cha kutamani kufuli hili lifunguke na tutoke nje.
Nikaivua bunduki yangu na kuikoki vizuri, nikasimama vizuri huku nikilitazama kufuli hili. Nikaanza kufyatua risasi risasi zisizo na idadi katika hili kufulia, cha kushangaza kufuli halikufunguka wala kutetereka.
“Dany”
Vivian aliniita kwa sauti ya unyonge huku akinishika, begani nikamgeukia uso wake unaonyesha kuna kitu kimetokea, ikanibidi kugeuka nyuma yangu. Nilihisi kuanguka na kupoteza fahamu ila haipo hivyo. Joka lenye vichwa viwili limesimama mita chache kutoka sehemu tulipo huku likitutazama mimi na Vivian ambao hadi sasa hivi hatujui ni nini tufanye.
AISIIIII……….U KILL ME 80
Katika maisha yangu nilisha wahi kusika kwamba kuna majoka ya kutisha na kuogopesa, ila sikuwahi kuyaona zaidi ya kusikia stori au kutazama filamu za namna hiyo kama Anaconda. Mwili mzima ukaanza kusisimka, nguvu zikaniishia bumbuazi zito likanitawala. Kwa macho ya kuiba, nikamtazama Vivian, nikamuona akitetemeka hata kuliko mimi, jasho jingi linamwagika usoni mwake. Taratibu nikayafumba macho yangu na kiroho roho nikaanza kusali taratibu kwa Mungu wangu anisamehe zambi zangu zote nilizo zifanya kwa maana ni zambi nyingi sana. Kifo ninakiona mbele yangu, machozi yakaanza kunitiririka. Hata bunduki niliyo ishika mkononi mwangu ikaanguka chini. Kitu ninacho kisubiria kwa wakati huu, ni joka hili kunitafuna na iwe ndio mwisho wa maisha yangu.
Dakika takribani tano zikapita kukiwa na ukimya mzito, sikusikia kitu chochote ndani ya dakika hizi tano, nikaanza kujiuliza maswali ambayo taratibu yakanifanya niyafumbue macho yangu. Nikahisi kama ninaota ila ndio ninacho kiona. Joka ambalo lilikuwa mbele yangu halikuwepo, Vivian naye ameanguka chini. Nikatazama nyuma yangu ambapo kuna geti nililo kuwa ninasumbuka kuvunja kufuli lake kwa risasi, ila ninalikuta wazi.
Kwa haraka nikamsogelea Vivia, nikampima mapigo yake ya moyo, nikaona bado yanafanya kazi vizuri, nikamnyanyua Vivian na kumbeba mikononi mwangu. Kitu cha muhimu kwa wakati huu ni kutoka katika hii sehemu kwa maana hadi muda huu bado ninajiuliza ni kitu gani ambacho kimetoka hadi muda huu nipo salama, na joka hili limepotea wapi na geti limekuwaje likafunguka. Sikupata jibu la aina yoyote zaidi ya kutoka nje ambapo kuna mwanga wa mbalamwezi. Sehemu niliyo tokea ni pembezoni mwa bahari.
Nikaendelea kutembea kwa mwendo wa haraka huku nikiwa nimembeba Vivian mikononi mwangu, sikhitaji kuwa karibu kabisa na sehemu ambayo tumetokae kwa maana sielewi ni kitu gani kinacho weza kutokea katika wakati huu wa usiku. Nilipo hakikisha nimetembea umbali mrefu kutoka lilipo geti, pembezoni mwa fukwe hii iliyo tulia nikatafuta sehemu, taratibu nikamlaza Vivian ambaye hadi sasa hivi haelewi kitu chochote kinacho endelea.
Nikaanza kumpa huduma ya kwanza kwa mtu ambaye amepoteza fahamu. Nikamjaza pumzi mdomoni mwake kwa kutumia mdomo wangu. Ila hapakuwa na matokea yoyote.
“Usihangaike sana, ataamka”
Sauti ya kike ambayo sio ngeni masikioni mwangu, niliisikia ikizungumza nyuma yangu, na kujikuta nikisimama kwa haraka huku nikigeuka nyuma. Sikuamini kumuona OLVIA HITLER, akiwa amesimama nyuma yangu, huku amevaa mavazi meupe. Mara yangu ya mwisho kukutana na dada huyu wa kijini ni siku nilipo kuwa Tanga kwenye moja ya hoteli.
“Vipi umesyuka sana eheee?”
Kwa kigugumizi kilicho nishika kutokana na mstuko, wala sikuweza kumjibu chochote Olvia Hitler. Nikabaki nikiwa nimekaa kimya ninamtazama usoni mwake.
“Nilikuahidi kwamba ukihitaji msaada wangu, nitakusaidia, na hicho ndio kitu nilicho kifanya leo kwako”
“Kwa nini umenisaidia?”
“Kwa ajili ya maisha yako, na nitahitaji sasa urudi Tanzania”
“Nitarudije wakati sina chochote na hapa nilipo wala sitambui nipo sehemu gani”
“Kwa binadamu hicho kitu ni kweli hakiwezekani, ila kwetu sisi kinawezekana”
Olvia Hitler akapiga hatua moja mbele na kuwa karibu kabisa na mimi. Akamtazama Vivian ambaye bado hajitambui, kisha taratibu mikono yake akaipitisha shingoni mwangu na kusogea karibu kabisa na mimi na miili yetu ikawa imekutana.
“Naamini kwamba si mara ya kwanza kwa wewe kunisikia”
Olvia Hitler alizungumza kwa sauti ya chini sana.
“Ndio”
“Sihitaji kufanya kama nilicho mfanyia baba yako mkubwa Eddy”
“Uma maanisha nini?”
“Nahitaji kitu kimoja tu kutoka kwako”
“Kitu gani?”
“Mtoto na nitakusiaidi kurudi Tanzania na nitakufanyia chochote utakacho kihitaji. Ila ukishindwa kufanya hivyo basi utarudi ndani ya gereza ulilo toka”
Maneno ya Olvia Hitler yakanifanya nizidi kubaki nikiwa ninamshangaa. Hakuhitaji nimsubirie kumjibu kitu chochote alicho kifanya nikuanza kujinyonya lipsi zangu. Woga, wasiwasi, vyote vikaniondoka mwilini mwangu. Nikajikuta nikijiamini sana, hata msisimko wa mapenzi ukawa ni mkali kuliko hata ilivyo kwa wanawake wengine. Olvia Hitler akaanza kunivua nguo zangu taratibu huku tukisogelea maji ya bahari yaliyopo mbeni yetu. Kwa raha ambayo ninaisikia nikamnyanyua na kuanza kutembea naye kueleka kwenye maji ya bahari.
Tukaingia kwenye maji ambayo yanatufikia kiunoni. Olvia Hitler akalivua gauni lake juupe linalo meremeta sana. Kuna utofauti mkubwa sana kati ya kufanya mapenzi kati ya binadamu na jinni. Pezi la Olvia Hitler, siwezi kulifananisha na mwanamke wa aina yoyote, japo sijajua kitumbua chake kina utamu wa aina gani ila kusema ukweli kunyonyana kwetu tu, kuna raha sana.
Olvia Hitler akamshika jogoo wangu ambaye tayari amesha simama muda mrefu, akaanza kumchua taratibu. Mimi kazi yangu ikawa ni kuhakikisha ninacheza na kifua chake kwa kuyaminya maziwa yake kwa utaalamu ninao ujua mimi. Olvia hakusita kuporomosha vilio vya raha. Olvia taraibu akageuka na kuinama, akamuingia jogoo wangu kwenye kitumbua chake. Nilitamani kupiga ukelele mkubwa kwa raha ninayo isikia ila, nikajitahidi sana kuwa kimya. Ninafahamu ladha za vitumbua vya wanawake wengi, ila cha Olvia Hitler, sijui nikielezeeje. Joto si joto, kubana si kubana yaani ni raha mtindo mmoja.
Olvia Hitler akazidi kunionyesha kwamba yeye ni tofauti na binadamu, kwani kitumbua chake kadri muda iunavyo zidi kwenda ndivyo jinsi kinavyo leta ladha tofauti tofauti. Nikajihisi nipo dunia ya kwangu peke yangu, ila hata kuzungumza nikashindwa, kazi yangu ni kukichezesha kiuno changu ili jogoo wangu azidi kufaidi hii raha ambayo kwenye maisha yangu ndio ninaipata leo.
Waarabu weupe wakatoka na kuzama kwenye kitumbua cha Olvia Hitler, na kumfanya atoe mguno mlaini huku akitabasamu. Baada ya kuhakikisha waarabu wote wameingia kwenye kitumbua cha Olvia, akanyanyuka na kunigeukia, akanikumbatia kwa nguvu huku akininyonya midomo yangu.
“Dany umenipa kitu ambacho sikuwahi kupewa na binadamu yoyote”
“Hata mimi sijawahi kupata raha kama hii”
“Nashukuru kwa kiumbe ulicho niwekea tumboni kwangu”
Nikabaki kimya nikimtazama Olvia Hitler, wala sikufahamu nimjibu kitu gani.
“Twende ukavae nguo zako niwasaidie”
Tukatoka kwenye maji, na kuanza kuokota nguo moja baada ya nyingine. Nikavaa nguo zangu, hata Olvia Hitler naye akavaa gauni lake, cha kushangaza ndani ya muda mchache likakauka maji. Akamsogelea Vivian na kumshika na kiganja cha mkono wake wa kulia kwenye paji la uso wake. Kwa haraka Vivian akakurupuka kutoka usingizini.
Alipo muona Olvia Hitler akaanza kuhema kwa nguvu huku akiwa amemkazia macho. Aakataka kusimama ila Olvia Hitler akamuwahi kumkalisha chini.
“Tulia Vivian”
“Kwani unamfahamu?”
“Ni rahisi kwangu kumfahamu, ila ana niogopa kwa maana aliniona nikipambana na lile joka”
Hapa ndip nikafahamu kwamba Olvia ndio amepambana na joka lile lililo kuwa likihitaji kutushambulia mimi na Vivian. Olvia Hitler akamshika mkono wa kulia Vivian na kumvuta kutoka chini alipo kaa na kumnyanyua.
“Umewezaje kuliua lile joka?”
Vivian aliuliza kwa sauti ya unyonge sana
“Usijali nitakueleza baadae cha msingi hapa ni kuondoka haraka iwezekanavyo”
“Kwani unalifahamu hili eneo”
“Yaa na hapo mbele kuna gari langu nimeliacha tuondokeni”
Tukaanza kutemebea kwa mwendo wa haraka huku tukimfwata Olvia Hitler kwa nyuma. Tukafika kwenye marabara ya lami ambayo imetulia sana. Kwa mbali kidogo tukaona gari lenye rangi nyeusi likiwa limesimama. Olvia Hitler akaendelea kutangulia mbele huku sisi tukifwata nyuma hadi kwenye gari lake.
Kabla ya kuingia kwenye gari, akanitazama mkononi mwangu kwenye bandeji ambalo niliingizwa kitu fulani siku ambayo ninaingia kwenye lile gereza.
“Vivi ingia kwenye gari mwaya”
Olvia Hitler alizungumza huku akimfungulia mlango Vivian. Baada ya Vivian kuingia kwenye mlango na kuufunga mlango, Olvia Hitler akaushika mkono wangu wenye bandeji, cha kushangaza bandeji hilo ambalo ni gumu, likalegea na kuvuka mkononi mwangu. Kivaa nilicho ingizwa ndani ya mwili wangu akakitoa kwa jinsi anavyo jua yeye na wala sikusikia maumivu ya aina yoyote. Sikuona jeraha lolote akakitupa kifaa hicho kidogo, kisha tukaingia kwenye gari.
Akawasha gari na taratibu tukaanza kuondoka katika eneo hili, huku kila mmoja akiwa haamini kama amesalimika kutoka katika gereza hili ambalo linatisha na lina manyanyaso makubwa sana.
“Vivi umafahamu mmiliki wa lile gereza tulilo kuwepo?”
“Hapana”
“Umeishi kwa kipindi gani kwenye lile gereza?”
“Ni kwa kipindi kirefu, inaweza kufika hata miaka mitano, niliingia pale nikiwa binti mdogo sana”
“Mutaka kumfahamu mmiliki wa hilo gereza?”
Swali la Olvia Hitler likatufanya mimi na Vivian kukaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha mimi nikajibu.
“Ndio tunahitaji”
“Ila Dany wewe hupaswi kumfahamu”
“Kwa nini?”
“Tutazungumza zidi tumifika hotelini”
“Sawa”
Nikabaki kimya huku nikijiuliza ni kwa nini Olvia Hitler aliamua kuniambia hiyo. Hatukuchukua muda mwingi tukafika kwenye moja ya jengo kubwa la hoteli, akasimamisha gari pembeni sote tukashuka, na kuelekea ndani. Muhudumu aliyopo mapokezi akatabasamu baada ya kumuona Olvia.
“Madam ndio unarudi?”
“Yaaa, hembu nipatie kadi yangu”
“Sawa”
Muhudumu akageuka nyuma yake amapo kuna sehemu ya kuhifadhia hizo kazi, akachomoa kadi moja na kumkabidhi Olvia Hitler
“Hawa ni wageni wangu”
“Ahaa sawa jamani karibuni”
“Asante sana”
Tukaelekea hadi eneo lililo na Lifti. Tukaingia ndani ya lifti hii, iliyo tupelekea hadi gorofa ya nane, ikasimama na kutoka ndani ya lifti. Tukatembea kwenye kordo hii ndefu hadi chumba cha sita kwa upande wa kulia kwetu. Olvia akasimama kwenye mlango huo, kwa kutumia kadi hiyo ya kufungulia milango akafungua mlango, ukafunguka na akatukaribisha ndani sote.
“Tutakaa hapa kwa muda kabla ya kurudi Tanzania”
“Sawa”
Katika chumba hichi kikubwa, kina chumba kingine ndani cha kulala, na hapa tulipo simama ni sebleni.
“Dany ninakuomba”
Olvia Hitler alizungumza huku akiingia ndani ya chumba cha kulala, nikamfwata kwa nyuma huku tukimuacha Vivian akiwa amekaa kwenye moja ya sofa kubwa lililopo kwenye hichi chumba. Olvia Hitler akachukua rimoti na kuwasha Tv, kisha akanigeukia na kunitazama machoni mwangu.
“Upo tayari kumfahamu mtu anaye miliki lile gereza?”
“Ndio”
“Huto kasirika?”
“Mmmmm wewe niambie tu”
Olvia akakaa kimya kwa muda huku akionekana akitafakari kitu cha kuzungumza na kunifanya nizidi kuwa na hamu ya kuhitaji kumfahamu mmiliki wa gereza ni nani.
ITAENDELEA
Post your Comment