Get the latest updates from us for free

mas template
Home » , » AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 19 na 20)

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 19 na 20)

Written By Bigie on Saturday, March 3, 2018 | 10:11:00 AM

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA 
ILIPOISHIA  

“Ni upumbavu mulio fanya, munge muua. Sasa hii ni nafasi ya mwisho jifiche kwenye hiyo bustani wanarudi muda si mrefu. Sasa ole wako ufanye makosa nitakuua”
Maneno ya Yudia yalinifanya niishiwe nguvu kabisa kwa maana yale mawazo mabaya niliyo kuwa nina muwazia kumbe ni kweli na yeye ndio anahusika na mpango wa mauaji ya mama, nikatamani kuingia ila nilihisi kushindwa kabisa kwa maana jamaa huyo amejificha katika uwa kubwa lililopo kwenye bustani iliyopo karibu na getini na yoyote atakaye ingia ndani hapo ni rahisi kumuona ila mtu anaye ingia si rahisi kuweza kumuona muuaji huyo.

ENDELEA   
Nikashusha pumzi na kujiweka sawa huku macho yangu yakichungulia getini, nikamuona Yudia akiingia ndani na kuufunga mlango.  Nikasimama getini kama dakika mbili nikitafakari nini cha kufanya, nikautazama ukuta wa nyumaba yetu, kusema kweli siwezi kuupanda kwa maana juu umewekwa nyaya za umeme ambazo endapo mtu atapanda basi atakacho kutana nacho hapo ni shoti ya uhakika ambayo inaweza kupelekea hata akapoteza maisha. 
 
Kutokana leo haturudi nyumbani, moja kwa moja nikaondoka getini na kurudi kwenye baa ambayo niliacha gari, nikaingia kwenye gari na kuitoa simu yangu mfukoni na kuanza kukagua taarifa alizo nitumia Joseph. Nikatoa na hati ya kusafiria ya gaidi niliye muua kwenye hoteli ya Tanga Beach Resort, hapo ndipo nilipo gundua kwamba kuna kikundi kikubwa cha hawa magaidi kimeingia hapa jijini Tanga. Kwa maana niliye muua na huyu niliye tumiwa taarifa zake pamoja na picha yake ni watu wawili tofauti.
‘Sasa raisi anakuja Tanga inakuwaje?’   
Nilijiuliza swali huku nikiendelea kutazama hati ya gaidi niliye muua. Nikatafuta namba ya Joseph kwenye simu yangu na kumpigia, simu yake ikaita kwa muda kisha akapokea.
“Dany niambie”
 
“Poa hivi umesema raisi anakuja Tanga?”
“Ndio na tayari jamaa wamesha tumwa kuweka mazingira sawa”
“Nani ni mkuu wa upelelezi aliye fika Tanga?”
“Mzee Haule ndio anaongoza upelelezi na ulinzi mzima wa raisi”
“Ok nipatie namba yake niwasiliane naye, kwa maana kuna mfumo mbaya unakwenda kutokea”
“Vipi kuna hali yoyote ya hatari?”
“Ndio, nitumie namba yake niweze kuzungumza naye”
“Ok dakika moja ndugu yangu”
Nikakata simu na kuisubiria meseji ya Joseph, haikupita hata dakika meseji ikaingia kwenye simu yangu, nikaifungua kwa haraka na kukuta namba ya simu ya Mzee Haule, kwa haraka nikaipiga namba hiyo ya simu ambayo ikaita kwa muda kisha ikapokelewa na nikasikia sauti nzito yam zee huyo ambaye ninamfahamu kwa kumuona.
 
“Shikamoo mkuu”
“Marahaba, nani mwanzangu?”
“Unazungumza na Agent Daniel 008 kutoka kitengo cha N.S.S”
“Ndio”   
“Nipo mkoa wa Tanga kwa sasa likizo ila nina taarifa muhimu ambazo ninahitaji kuweza kuzileta kwako”
“Upo wapi kwa sasa?”
“Nipo maeneo ya Chumbageni”
“Ok unaweza kufika maeneo ya Tanha Hoteli hapa hapa Chumbageni”
“Kwenye hiyo hoteli?”
“Ndio”
“Dakika tatu nitakuwa hapo”
 
Nikakata simu na kuwasha gari, nikaondoka katika eneo hili, kutokana sio mbali sana na sehemu nilipo kuwepo, ndani ya dakika tatu nikawa nimesha fika katika eneo hilo. Nikashuka kwenye gari na kutoa simu yangu nikampigia mzee Haule aliye toka nje ya hoteli hiyo, akaingia kwenye gari langu na nikaanza kumpa taarifa muhimu sana za kuimarisha ulinzi.
“Ina maana wewe ndio uliye weza kumuua yule gaidi kule hotelini?”
“Sikumuua ila alijiua mwenyewe kwa kuhofia kutoa siri za watu wanao walio mtu hiyo kazi. Na hivi ndio vitu ambavyo niliweza kuvipata kama vidhibitisho”
Mzee Haule akapokea hati ya kusafiria ya gaidi huyo pamoja na waleti ambayo nilimpatia nyenye vikara vilivyo andikwa kwa lugha ya kiarabu. Mzee Haula akaanza kuzivizsoma, sura yake nikaona jinsi inavyo badilika, sikujua kama anaweza kuelewa lugha hiyo.
 
“Pumbavu sana”
“Kuna nini mzee kwa maana nimeshindwa kusoma hayo maandishi?”
“Wana mpango wa kuzuia bandari mpya kujengwa, pili wana mpango wa kuzuia msafara wa raisi usiweze kuja hapa”
“Sasa tunafanya nini mkuu?”
“Hii kazi niachie mimi na vijana wangu tunakwenda kuikamilisha”
Nikataka kumueleza Mzee Haule juu ya nyaraka zilizo ibiwa nyumbani kwa mama ila nikashindwa kufanya hivyo kwa maana hiyo ni ishu yangu mimi mwenywe.
“Nipo na meya hapa ninamalizia kufanya mkutano mdogo wa maandalizi ya kuja kwa raisi, wewe nenda kapumzike tu nyumbani”
Alipo sema yupo na meya, nikahisi mapigo ya moyo kuanza kuniaenda mbio, ila nikajikaza kuto kuonyesha mstuko wowote, kwani tayari imani na mzee Haule imesha anza kunitoweka.
 
“Sawa mkuu”   
Akashuka kwenye gari huku akiwa amebeba waleti hiyo pamoja na vikaratasi vyote, nikabaki nikimtazama anapo kwenda, nikamuona akikaa kwenye moja ya meza ambapo kuna watu wawili wamekaa, mmoja akiwa ni mzee mzee ila huyu wa pili ni mtu ambaye Joseph alinitumia picha yake na taarifa yake.
“Kumbe huyu naye ndio wao”
Nikageuza gari na kulisimamisha sehemu ya mbali kidogo na hoteli hiyo kisha nikaanza kutembea kwa miguu hadi katika hoteli hiyo, safari hii nimerudi kwa kazi moja tu ya kupeleleza ni nini mzee Haule anakifanya na meya huyu pamoja na mtu ambaye anashirikiana na Yudia mfanyakazi wetu wa ndani. Nikamuona mzee Haule akimkabidhi jamaa huyo wallet ambayo ninaamini kwamba nimeitoa gaidi niliye muua. Nikaitoa simu yangu, na kaunza kuwapiga picha za siri sana pasipo wao wenyewe kuweza kujua kwamba ninawapiga picha, nilipo hakikisha kwamba nimemaliza kufanya hivyo kwa haraka nikaondoka katika eneo hilo, nikarudi kwenye gari na kumpigia mama simu.
 
“Mama naomba unitumie picha ya huyo meya”
“Vipi umekwenda kwake?”
“Hapana wewe nitumie tu hiyo picha”
“Sawa, nakutumia Whatsapp”
“Ok”
Nikakata simu na kuisubiria picha hiyo ya mama anayo hitaji kunitumia. Mama akaituma picha ya meya huyo kwenye simu yangu, nilipo ifungua, nikawa na uhakika kwamba ndio mzee niliye muona anazungumza na mzee Haule ambaye tayuari nimesha tambua kwamba anashirikiana na Meya huyo. Mtu pekee ambaye nimebakisha kumuamini katika kuifanya kazi hii ni K2, mkuu wa kitengo changu. Ikanilazimu kuweza kumpigia simu, nikaanza kumuelezea kila kitu ambacho kinaendelea kwa sasa na hali inavyo elekea kwa sasa kwamba raisi wan chi yupo katika hali ya hatari sana.
“Dany sasa sikia, sasa hivi ninawatuma Godfrey na Lukas, waanze safari kuja Tanga, hakikisha kwamba kazi hii munaifanya kwa usiri sana, na raisi mimi nitaambatana naye kwenye msafara wake kesho kutwa”
 
“Sawa bosi”
“Sipendi unite bosi Dany”
“Sawa honey”
“Poa makini mpenzi wangu”
“Nipo makini baby”
“Ok”
Nikarudi hotelini hapo na kusimamisha gari langu kwa mbali kidogo kwa ajili ya kuweza kuona ni kitu gani kinacho endelea. Haukupita muda sana meya huyo akatoka akiwa amongozana kijana wake. Wakaingia kwenye gari lao aina ya Voxy na kuondoka eneo la hotelini hapa. Taratibu nikaanza kuwafwatilia huku nikiwa makini sana kuhakikisha kwamba hawanistukii. Gari hiyo y Meya inayo endeshwa na kijana huyo, nikaiona inaingia kwenye moja ya jumba la kifahari maeneo ya Sahare. 

Geti la jumba hilo likafungwa kwa haraka nikashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu hadi kwenye ukuta wa jumba hilo, nilipo uchunguza vizuri nikaona ukuta huo kwa juu una chupa chupa ndogo tu na si nyaya za umeme. Nikaichomo bastola yangu nikaikagua magazine yake, risasi zilizo kuwemo ndani ya magazine hiyo zinatosha kunilinda kwa chochote kitakacho nitokea cha hatari. Nikaichomeka kiunoni kwa nyuma, kisha nikarudi nyuma hatua kama kumi, kisha nikaanza kukimbia kwa kasi kuufwata ukuta huo. 

Nikakanyaga mara mbili kwa kasi katika ukuta huo na kujishikiza kwa juu. Haikuwa kazi ngumu mimi kuweza kufanya hivyo kwa maana kipindi nipo kwenye mafunzo maalumu ya upelezi kuruka ukuta ilikuwa ni moja ya zoezi nililo kuwa nikilifanya kiufasaha sana. Nikajivuta kwenda juu taratibu na kuchungualia ndani ya jumba hilo. Nilihisi kuzimia, kwa maana kikosi cha watu wasio pungua chini ya thelathini wenye bunduki zao na vilemba kichwani wamejipanga kwenye mistari mitatu yenye watu kumi kumi.
Meya yeye na kijana huyo ambaye ni gaidi kutoka katika kundi la Al-Shabab wana kazi ya kuwakagua vijana hao, ambao wanaaonekana wamekamilika katika maswala ya kivita. 

Taratibu nikaning’inia kwa mkono mmoja huku mwengine ukitoa simu yangu, nikapiga picha mbili za haraka pasipo wao kustukiwa, kisha nikashuka kwenye ukuta huo taratibu, nilipo hakikisha nimekanyaga chini nikaanza kutembea kwa hatua za kasi hadi mbali kidogo mwa nyumba hiyo. Nikapiga sicha nyumba hiyo kwa mbali kisha nikaingia ndani ya gari na kuanza kurudi nyumbani kwa mama na safari hii kazi ni kumfwata Yudia, na yeye ndio nitakaye mminya na kunieleza kila kitu. Saa yangu ya mkononi inaonyesha ni saa tano kasoro usiku, kichwani mwangu mawazo mengi yalinitawala.
Picha zote nilizo zipiga kuanzia hotelini na kwenye jumba hilo lililo ficha kikosi hicho cha magaidi nikamtumia K2, na ndani ya dakika moja akanipigia simu.
“Dany ina maana hichi kikundi kipo hapo Tanga?”
“Ndio honey”
“Mungu wangu, ngoja nimtumie RPC, wa mkowa huo pamoja na mkuu wa mkoa”
“Sawa utakuwa umefanya la maana pasipo kufanya hivyo, kesho kutwa ni damu za watu wengi zinaweza kupotea”
“Sawa natuma sasa hivi”
 
K2 akakata simu akionekana kuchanganyikiwa. Bastola yangu nikaiweka katika siti ya pembeni, safari hii nikiwa nimejipanga kwa lolote litakalo jitokeza hata yule mpumbavu aliye jificha kwenye ua la nyumbani kwetu akitarajia kumuua mama basi hana bahati katika siku yake ya leo. Nikafika nyumabi getini, bastola yangu nikaishika na mkono wa kushoto, nilipo hakikisha kwamb nimesha iweka ayari, nikapiga honi kwa nguvu huku taa za gari nikiwa nimezizima. Nikasikia geti likifunguliwa kwa ndani, kisha likafunguliwa na Yudia aliye valia suruali ya kubana na tisheti iliyo ubana mwili wake. Taratibu nikayatupia macho kwenye ua alilo jificha mtu wa Yudia, kutokana nilimuona mara ya kwanza alipo jificha hata wakati huu niliweza kumuona jinsi alivyo jibanza. Nikamtazama Yudia aliye simama pembeni ya geti akisubiria kuliingiza gari.
 
    Kwa kasi ambayo hata Yudia mwenywe hakuitegemea, nikaingiza gari huku nikiwasha taa na kuelekea kwenye ua hilo. Mtu wa Yudia alipo ona nimemlenga na gari kwa haraka akajirusha pembeni, Hata kabla gari hajasimama nikafungua mlango na kujirusha nje nikiwa na bastola mkononi mwangu. Mtu huyo niliye mpotezea umakini wa kunishambulia, alibabaika katika kuitafuta bunduki yake alipo angukia. Sikuwa na huruma hata kidogo, nikaanza kumpatandika risasi kadhaa katika mwili wake zilizo pelekea maisha yake kuishia hapo. Yudia getini alishikwa na bumbuazi naamini hakuweza kujua kama ninaweza kufanya kitu cha namna hiyo. Kwa haraka nikamfwata getini na kulifunga geti kwa ndani kwa maana nina amini milio ya risasi ni lazima iwastue majirani zetu.
 
“Ingia ndani”
Nilimuambia Yudia kwa ukali, akastuka na kutoka katika bumbuwazi lake. Nikamshika mkono na kuanza kumvuta huku nikimpeleka ndani. Nikamsukumia kwenye sofa huku nikiwa nimemuelekezea bastola.
“Wewe ni nani?”
Yudia macho yalimtoka huku jasho jingi likimwagika. Nikarudia tena kumuuliza kwa ukali tena safari hiii nikiukaza mkono wangu ulio muelekezea bastola hiyo, nikiashiria kwamba sitanii kwa kile kitu ambacho nina kizungumza kwa muda huu.
Taratibu nikakiona kifua cha Yudia jinsi kinayo tuliza mapigo ya moyo taratibu, akanyanyuka kwenye sofa kwa kujiamini na kunifanya nirudi nyuma hatua kadhaa ili hata akihitaji kuni shambulia basi iwe raisi kumuwasha bunduki.
 
“Nashangaa sana mwanaume anaye jiamini kumshikia mtoto wa kike mzuri kama mimi bastola”
Maneno ya Yudia yalinishangaza sana kiasi cha kunifanya nizidi kupandwa na hisira kwa maana yamejaa kejeli kubwa ndani yake.
“Kama ni mwanaume kweli unaweza kuweka bastola yako chini na kuupanga mkono, ila kama hujiamini basi unaweza kunipiga risasi nife”
‘Anajiamini nini huyu mtoto?’s
Nilijiuliza huku nikimtazama Yudia kuanzia chini hadi juu, kutokana nina jiamini katika swala la mapambano, nikaona haina haja ya mimi kumpiga risasi Yudia kwa mana nina hitaji taarifa za muhimu kutoka kwake. Nikaitoa magazine kwenye bastola yangu na kuirushia kwenye sofa jingine huku bastola yangu nayo nikiiweka kwenye sofa jingine. Nijajiweka swa huku nikikunja ngumi tayari kwa kupambana na Yudia, ila gafla Yudia akachomoa bastola kwenye kiuno chake aliyo kuwa aneificha pasipo mimi kuiona. Akanielekezea huku akiachia msunyo mkali na kuzungumza manoeno ya kejeli.
“Fala mkubwa wewe, unakwenda kufa kifo cha kidada kama hichi, na baada ya hapo yule Mbuzi mama yako ndio anakwenda kuftwatia”
                                                                                         
       AISIIIII……….U KILL ME 20

   Nilibaki nikiwa nimemkazia macho Yudia kusema kweli hata akitokea mama kwa muda huu hatoweza kuamini kwamba Yudia, binti anaye onekana ni mnyonge na mpole ndio huyu ambaye amenishikia bastola hapa. Sikuwa na jinsi yoyote zaidi ya kuwa mnyonge ila nikizidi kumsoma ni kwa umakini ni kitu gani ambacho atakwenda kukifanya.
“Vua nguo zako”
Yudia aliniamrisha kwa sauti ya ukali sana, sikutarajia kama anaweza kuzungumza kwa ukali kiasi hicho. Japo nilisha mtilia mashaka kuanzi mwanzo ila sikudhani kwamba ni mkali kwa kiasi hichi. Akarudia kuzungumza kwa ukali, hapo sikuwa na unjanja ikanibidi kutii kitu anacho kizungumza, nikaanza kuvua nguoa moja baada ya nyingine, nikianzia na shati, suruali  na nikabakiwa na boksa. Kwa ishara akanionyesha niivue boksa yangu, nikafanya hivyo na kubaki mwepe kama nilivyo zaliwa.
 
“Waooo big cock”   
Yudia alizungumza huku akimtazama jogoo wangu. Akanitazama kuanzia juu hadi chini huku bastola yake akiwa bado amenielekezea mimi.
“Nakupa machaguo mawili, ukikubali maisha yako yatakuwa salama. Ukikataa basi unarudi ardhini”
“Machaguo gani?”
Nilimuuliza Yudia kwa sauti yenye mitetemesho mizito ya hasira, nikitamani sana kumshambulia Yudia kwa maana kitu anacho kifanya ni udhalilishaji mkubwa sana kwangu.
“Moja nahitaji unile, ukishindwa ninakuua. Ukishindwa hilo nitahitaji unieleze ni wapi alipo mama yako”
Chaguzi la kwanza kwangu ni rahisi sana kwangu, ila la pili ni gumu sana kwa maana nimesha tambua kwamba adui wa kwanza kwa mama yangu ni meya na vibaraka wake mmoja wapo ni Yudia.
 
“Nachagua namba moja”
Nilizungumza kwa kujiamini, Yudia akaachia tabasamu pana na kunanza kuvua nguo zake moja baada ya nyingine huku akiwa ameninyooshea bastola yake. Alipo bakiwa na bikini yake, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu huku bastola yake akiwa bado ameishika. Tukaanza kunyonyana denda huku mikono yangu kiwa inayaminya makalio yake niliyo kuwa nikiyatamani sana kunyaminya. Nafanya yote haya kwa sababu ya kumuokoa mama yangu ila kitu kingine ninacho kiwaza ni jinsi miulio ya risasai ilivyo sikika kwa majirani zangu, nina imani watakuwa wamewajulisha askari juu ya tukio hilo. Sikutaka kabisa Yudia nimuendee kwa papara, kwa maana kufanya hivyo inaweza kuhatarisha maisha ya mama yangu ambaye siku zote alikuwa akiishia naye kumbe ana mpeleleza, na hadi sasa hivi sitambui ana fahamu mambo mangapi ya mama yangu.
 
“Ohooo”
Yudia alitoa mguno baada ya kuzidi kuyaminya makalio yake huku nikiyagawanyisha gawanyisha. Njia moja na rahisi ya kuweza kumtambua Yudia, nikufamu kujua ni wapi hisia zake zilipo, nikifanikiwa katika hilo basi ninaweza kumuuliza kitu chochote na anaweza akanijibu pasipo kipingamizi. Nikaanza kuyanyonya maziwa yake huku nikiwa nimeyabananisha.
“Oooho Dany”
Nikazidi kunayonya kwa utaalamu ambao unaweza kumpagawisha Yudia. Yudia naye hakuwa nyuma japo mkono wake mmoja ameshika bastola ila mkono wake mwingine ukashika jogoo wangu na kuanza kumchua taratibu. 
 
Nikamuinamisha na kumshikisha meza, akaniachia makalio yake niliyo anza kuyatia makofi taratibu huku nikisogeza kijimkanda cha bikinini aliyo vaa. Jogoo wangu nikampaka mate ya kutosha na taratibu nikamsokomeza kwenye kitumbua chake. Nikavuta pumzi ya kutosha, kisha nikaanza kasi ya kuishambulia ikulu yake huku nikiwa nimeibana pumzi yake. Yudia akaanza kutoa vilio vya maaba ila bastola yake hakuwa tayari kuiachia hata kidogo. Nikazidi kumpeleka mpute mpute nikihisi anaweza kuzungumza ninacho hitaji kukifahamu ila wapi, nilipo ona azunguzi kwa njia ya mimi kumpelekesha kasi ikanilazimu kumuliza maswali kwa mdomo.
 
“Wewe ni nani?”
”Wewe unahisi mimi ni nani?”
“Nakuuliza wewe ni nani?”
Nilimuuliza huku nikizidi kucheza na kitumbua chake nikitumia ujuzi wangu wote katika kula kitumbua hicho.
“Acha mbinu za kiseng** una hisi kwa kunitomb** nitazungumza”
Mameno hayo ya Yudia hayakunikatisha tamaa kabisa, nikazidi kuongeza maujuzi ya kila namna ila Yudia akuzungumza katu katu. Tukaanza kusikia geti likigongwa kwa nguvu, huku nje tukisikia ving’rora vya gari za polisi.
“Shiti……”
 
Yudia alizungumza huku akimchomo jogoo wangu kwenye kitumbua chake. Nikataka kumvamia ila alinistukia kitu ambacho nilihitaji kukifanya. Akaninyooshea bastola yeka huku  akianza kuokota nguo yake moja baada ya nyingine.
“Simama hivyo hivyo”
Yudia alizungumza huku akianza kuivaa suruali yake, kwa haraka nikamrukia na kumvaa Yudia na kumuangusha chini. Kazi ikawa ni kuparangana hapo chini, sikuamini kama Yudia anaweza kuwa na guvu za kushindana na mwanaume kama mimi kwa maana anaweza kunizungusha vya kutosha. Akanilaza chini huku mikono yangu yote akiwa ameikamata kwa nguvu sana. 

Akanitandika kichwa cha pua na kunifanya nijisikie maumivu makali sana. Nikajaribu kujibu kichwa hicho kwa kutaka kuuchomoa mkono wangu wa kulia alioa ukandamiza kwa mkono wake wa kulia sakafuni ila nikashindwa. Akanitandika kichwa cha pili na cha tatu mfululizo na kujikuta giza kubwa sana likinitawala katika macho yangu, huku kwa mbali nikimuona Yudia akisimama na kumalizia kuvaa nguo zake akiwa katika hali ya haraka haraka. Alipo maliza, nikamuona akichukua kitu fulani juu ya kabati hapo sebleni, kisha akatoka sebleni na kuondoka.
 
“Ohoo mvalisheni nguo”
Ni sauti ya kiume niliyo isikia ya watu walio weza kuingia sebleni, watu hao nilio weza kuwatambua ni polisi, mmoja wao akaanza kunitingisha kuangalia kama nipo hai au nimekufa. Kuwasikia ninawasikia, ila kuzungumza kidogo na kunyanyuka ndio shida.
“Amezimia huyu”
“Hembu leteni maji ya baridi kwenye friji”
Sikumuona hata mtu aliye kwenda kuchukua maji kwenye friji ila ndani ya dakika nikastukia maji hayo nikimwagiwa kwa nguvu kwenye uso wangu na kujikuta nikiurupuka na kukaa kitako. Nikakuta askari wanne wa kiume walio valia sare zao wakinitazama.
 
“Yupo wapi Yudia”
Niliuliza huku nikisimama, sikujali kama nipo uchi, ila askari wawili wakaniomba niweze kukaa kwenye sifa nitulie kwa maana nina vuja damu puani. Nilipo jishika puani na kuona nina damu, hapo ndipo nikajikuta nikitulia huku nikikaa kwenye sofa. Akaskari mmoja akavua koti lake na kunifunika kwenye sehemu zangu za siri.
“Huyo Yudia ndio nani?”
“Kuna binti ametoka humu ndani?”
“Huyo mfanyakazi wa mama?”
Askari huyo aliuliza swali hilo akionyesha dhairi kwamba ana mfahamu Yudia.
“Ndio”
“Yule alitufungulia geti nak kutoka nje akidai kwamba anaogopa”
“Nini?”
Nikataka kunyanyuka ila askari hao wakanizuia nisinyanyuke na nisitoke nje uchi, kwa maana watu walisha kusanyika huko nje wakitazama ni kitu gani kilicho tokea.
 
“Ohoo nimesha mpoteza”
“Umempoteza nani?”
“Yudia”
“Kwani wewe ni nani?”
Sikulijibu swali la askari huyo zaidi ya kumkata jicho kali, sikutaka kumjibu kitu chochote zaidi ya kumuomba askari mwengine nguo zangu. Nikaanza kuvaa moja baada ya nyingine nilipo hakikisha kwamba nimevaa vizuri, nikampa polisi huyo anaye onekana ni mkuu wa polisi wengine waliomo humu sebleni, kitambulisho changu cha kazi. Akakipitishia macho kwa dakika moja kisha akanirudishia kwa heshima.
“Bastola yangu ipo wapi?”
“Wee mpe bastola yake”
Mkuu huyo wa askari alizungumza na kumfanya askari mwengine kunipatia bastola yangu ambayo tayari walisha ichomeka magazine.
 
“Hakikisheni kwamba munampata huyo msichana na maelekezo mengine anayo RPC wenu sawa”
“Sawa mkuu”
“Ondoeni hiyo maiti kwa maana mimi ndio nimepiga risasi, kisha niachieni vijana wawili hapa na wengine muondoke nao, nahitaji nyumba hii kuweza kuwekewa ulinzi”
“Sawa”
Maagizo yangu hayakuwa na askari aliye weza kuyapinga japo tupo vitengo tofauti vya ulinzi ila kidogo nimewazidi vyeo hawa ndio maana wanaweza kusikiliza amri yangu ambayo nina izungumza. Nilipo maliza kutoa maagizo hayo nikaingia chumbani kwangu na kazivua nguo na kuingia bafuni nikiwa na hasira sana. Nikajiosha damu inayo toka puani mwangu ambayo ilisha anza kukata. Nikaoga mwili mzima huku nikiwa ninajilaani sana kwa kupenda kufanya ngono kulilo kutekeleza majukumu yangu ya kazi. 
 
‘Haitokuja kutokea tena kwenye maisha yangu’
Nilijiapiza kimoyo moyo huku nikiwa nijajipaka sabuni sehemu kadhaa za mwili wangu kasoro mgongoni kwenye jeraha la moto nilio ungua. Nilipo maliza kuogo nikarudi chumbani kwangu, nikafungua begi langu sikuona nguo ya maana ninayo weza kuivaa kwa maani nimekuja likizo kwa hiyo nguo nyingi nilizo zibeba ni zakisharo baro.  Nikafungua kabati na kutazama nguo zangu ambazo huwa zipo tu hapa nyumbani. Nikaona suruali moja nyeusi pamoja na tisheti nyeusi, nikazitoa na kuziweka kitandani. 
 
Nikafunga kabati, kisha nikaanza kuzivaa nguo hizo huku nikianza kuvaa nguo ya ndani. Nilipo maliza kufanya hivyo, bastola yangu nikaichomeka kiunoni na kuifunika na tisheti. Nikaitoa simu yangu kwenye mfuko wa suruali nyingine, nikakuta missed call za mama zipatazo kumi. Nikatambu tayari alisha pata taarifa ya maafa yaliyo tokea nyumbani, nikampigia simu, ikaita kidogo na kupokelewa.
“Kuna nini kimetokea Dany”
“Usijali mama tukionana nitakuambi”
“Nimeambiwa kuna jambazi umeuwawa hapo nyumbani?
Mama aliuliza kwa shauku huku akionekana kujawa na wasiwasi mwingi sana.
“Ndio mama kuna jambazi nimeweza kumuua, ila usiwe na shaka hii ni opaesheni ninayo iendeleza”
“Ohooo Mungu wangu, hujaumia?”
“Sijaumia mama nipo sawa”
“Na mtoto wa watu Yudia je?”
Hapo kidogo nikanyamaza kimya kidogo nikifikiria ni kitu gani nimjibu mama, nilipo hakikisha kwamba nimepata jibu la uhakika nikamjibu.
 
“Yupo salama usijali katika hilo mama”
Ilinibidi kumuongopea mama kwa maana bado ni mapema kumuweka wazi kwamba Yudia ni mtu ambaye yupo nyuma ya mpango mzima wa mama kutaka kuuwawa.
“Kuwa makini mwanangu”
“Sawa mama”
Nikakata simu na kumpigia K2, ambaye simu yake ilianza kuita, akapokea.
“Dany”
“Umeweza kuwasiliana na mkuu wa mkoa pamoja na RPC?”
“Ndio nimesha weza kuwatumia na hizo picha kabisa”
“Nitumie namba ya RPC”
“Dany haupo vizuri hii kazi nimesha wakabidhi watu”
“Nimekuambia nitumie namba hiyo”
Niluzungumza kwa ukali, nahisi hadi K2 mwenyewe alishangaa kusikia sauti kama hiyo, japo ni mkuu wangu wa kazi ila hapa ninatumia ukuu wa mahusiano nilio kuwa nao ndani ya moyo wake.
“Ok honey”
Nikakata simu na kutoka nje, nikakuta tayari polisi wamesha utoa mwili wa jambazi huyo niliye weza kumua. Askari wengine wawili waliweza kubaki hapo nyumbani kwa kuweka ulinzi, nikaingia ndani ya gari ambalo kidogo kwa mbele, limebonyea. Taratibu nikaondoka nyumbani, huku akilini mwangu nikimuwaza Yudia.
 
“Fu**k me”
Nilijitukana kwa maana kumuacha Yudia huru itanigarimu sana kwenye maisha yangu, ila nikiwa njiani nikapata wazo na ikanibidi kugeuza gari langu kwa haraka na kurudi nyumbani lengo langu kubwa ni kwenda kutaza chumba cha Yudia kama kuna kitu chochote kinacho weza kunipa muongozo wa kuweza kumkata. Nikasimamisha gari pembeni ya ukuta wa nyumbani kisha nikashuka kwa haraka na kuanza kukimbilia getini, nikafungua geti na kuingia ndani. Sikuamini macho yangu kuwakuta wale askari ambao niliwaacha muda mchache tu ulio pita. Sasa hivi wote wawili wamelala chini wakiwa wanavuja damu ikionyesha kwamba wameuwawa. Nikiwa katika kushangaa shangaa, mlango wa kuingilia sebleni ukafunguliwa, uso kwa uso nikakutana na Yudia aliye shika begi lake mkononi akionekana yupo kwenye harakati za kutoroka huku nyumbani kwetu
 
  ITAENDELEA

Advertisement
hapa

Post your Comment

Habari Mpya